Tahajudi Kila Siku
Tayari tumeshaanzisha Tahajudi za pamoja za kila wiki kila Jumamosi saa 20:00 GMT kama inavyoonekana kutoka makala hapo chini. Hata hivyo, kwa kuwa idadi yetu imeongezeka kwa kasi Uongozi wa Kiroho sasa wanapendekeza kwamba sisi tuanzishe muda ambao kila siku makundi makubwa ya watu wanaweza Kutahajudi kwa pamoja.
Kila mtu ana njia zao wenyewe ya kuwa na msukumo – iwe ni Kutahajudi peke yake, kutahajudi kwa pamoja au mkutano ya pamoja mahali maalumu. Tumesema kila wakati jinsi Tahajudi inakuwa na nguvu zaidi kama ikifanyika kwa wakati mmoja. Katika mabara mbalimbali hata hivyo inahitaji kuwa wakati muafaka kwa watu wengi.
Kutokana na mawasiliano haya sisi tunapendekeza yafuatayo: kwamba Initiate wanatoa kipaumbele kipindi cha Kutahajudi kama saa moja kila siku ambayo inaanza wakati huo ulioonyesha hapa chini. Tafadhali msiichukulie hii kama mahitaji lakini kama nafasi ya kufanya kazi kwa pamoja kama sehemu ya timu ya wa kutuma na kueneza Mwanga na Sauti. Kwa kufanya kazi pamoja tutaongeza athari nzuri ya Nguvu za Kiroho kwenye Sayari na wakazi wake.
Saa zilizotajwa hapa chini ni za ndani ya nchi iliyotajwa.
Marekani Kaskazini
20:00 Kalifornia
20:00 Arizona
22:00 Chicago
22:00 Mexico
23:00 New York
Marekani Ya Kati na Kusini
21:00 Cuba
20:00 Peru
20:00 Colombia
20:00 Panama
21:00 Jamhuri Ya Dominika
21:00 Bolivia
21:00 Chile
22:00 Argentina
22:00 Brazil
Ulaya na Afrika
21:00 U.K.
20:00 Ghana
21:00 Ujerumani
21:00 Ufaransa
21:00 Spania
21:00 Uholanzi
21:00 Italia
22:00 sweden
23:00 Finland
22:00 Namibia
22:00 Afrika Ya Kusini
23:00 Kenya
23:00 Tanzania
Asia
20:00 India
22:30 Hong Kong
Australasia
19:00 Australia Magharibi
21:00 Australia Mashariki
23:00 New Zealand
Tunapenda kumkaribisha mtu yeyote ambaye anatahajudi, hata kama yeye sio mmoja wa kundi la Mwanga na Sauti, kutahajudi nasi kwenye saa hizo hapo juu. Kama nchi yako haionekani hapo na unahitaji msaada wa kufahamu wakati sahihi, tafadhali tujulishe kupitia ukurasa mawasiliano.
Tahajudi za Kila Wiki
Kama sehemu ya hoja ya jumla kuelekea kuwajali wengine tungependa Tahajudi za mara kwa mara ambazo zinafanyika kila wiki. Kwa wote kuwa pamoja kwa muda wa dakika 10 kwa wakati mmoja. Hii itakuwa taarifa ya nguvu kutoka kwenu kuthibitisha positivity kwa sayari kwa ujumla. Katika kufanya hivyo mtahisi uhusiano mkubwa kati yenu.
Idadi yetu imeongezeka kwa kasi cha ajabu katika kipindi cha miezi michache iliyopita, sasa tunao zaidi ya watu 200 waliofikia Enlightenment ya Kiroho.
Misheni yetu ni wa aina mbili, kwa Watahajudi kufikia Hali za juu za Kiroho na kuongeza Ufahamu wa Sayari. Kwa kuwa sasa tuna kundi kubwa la watu walioanzishwa kwenye Mwaanga na Sauti ni wakati wa kuunganisha na kutumia uwezo huu na kuandaa Tahajudi za wakati mmoja Dunia nzima.
Sisi ni kupendekeza kwamba hii ifanyike kila mwishoni mwa wiki. Awali, kutuma Upendo na Amani kwa Sayari na wakazi wake kwa muda wa dakika 10. Ukitaka kuongeza muda huu ni sawa lakini hakikisha unaanza kwa wakati sahihi kwa eneo lako. Angalia hapa chini.
Ingawaje hii ni kwa ajili ya Initiate wa Mwanga na Sauti sisi tunawakaribisha Watahajudi Duniani kote wajiunge nasi katika misheni yetu. Wengi wetu wanataka mabadiliko – hatimaye tuna uwezo wa kukamilisha hili – hebu tutumie vizuri fursa hii ya ajabu
Saa Za Kutahajudi Duniani Kote
Tafadhali kumbuka: saa hizi zinalenga 20:00 G.M.T. Jaribuni kuhakikisha muda wa nchi au mahali ulipo kwa makini na marekebisho yoyote ya muda wa Summer.
Jumamosi
13:00 Los Angeles
13:00 Phoenix
16:00 New York
15:00 Bogota
15:00 Lima
16:00 Santo Domingo
16:00 Santiago
17:00 Brasilia
21:00 London
22:00 Roma
22:00 Madrid
23:00 Helsinki
22:00 Windhoek
22:00 Pretoria
23:00 Dar es Salaam
Sunday
01:30 New Delhi
06:00 Brisbane
08:00 Wellington
Mara kwa mara tuna uwezekano wa kupata habari mpya kuhusu hizi Tahajudi kutoka kwa Uongozi wa Kiroho. Maelekezo yote mapya yataonekana hapa, hivyo kumbuka kuangalia na kusoma mara kwa mara.
Ushuhuda (F.A.)
Ushushaji mkubwa, wenye ‘upendo kwa mfumo wa uponyaji,’ kwa namna fulani; kwa ajili yangu binafsi na kwa binadamu kwa pamoja. Niliweza kuhisi ‘kujeruhiwa’ kwa binadamu, na kutokuwa na hatia kwa kujeruhi huko – ingawaje uzoefu wake tunauona kwa njia zisizovumilika. Kiini cha ufunuo huu tu ni, Mungu kurudi Kwake Mwenyewe kwa mabilioni ya njia – ili kutufunulia tu jinsi tunavyogawanyika, kuwa watu binafsi, kufanya msimamo wetu binafsi, na tukiwa tayari, kuyeyuka tena kurudi tulipotoka. Kile kinachohitajika ni kujitolea, kuwa wazi, kutoa kile tunachopokea, na kuimarisha Utambulisho wa Kiroho.