Makala hapa chini ni neno kwa neno, ni masahihisho tu ya spelling pamoja na vituo vya uandishi sahihi vimeongezwa. Ujumbe wa hivi karibuni huonekana juu ya ukurasa.
3 Februari 2023
Huyu ni Patrick.
Ni Ujumbe wangu wa mwisho kwako kwa muda tunapoendelea na Mafundisho ya Kiesoteric kama ilivyotajwa hapo awali.
Tunahitaji kueleza zaidi kuhusu maisha kwenye Sayari zingine katika ‘Malimwengu’ mengine, ili uwe na picha kamili ya kile kinachoendelea, badala ya ukweli nusu. Kuna mengi ya kujifunza juu ya somo ambalo limevutia watu kwa muda mrefu.
Mchakato wa “Ascension” ambao Tumewapitisha umemaanisha kuwa mamilioni ya watu sasa wako tayari Kuunganishwa na Viumbe walioendelea sana kutoka kwa ‘Walimwengu’ hawa kwa manufaa ya pande zote mbili.
28 Januari 2023
Huyu ni Patrick.
Kuna Ukweli fulani wa kimsingi ambao watu wengi hawaelewi kikamilifu. Hii inaeleweka kwani ni ngumu kufahamu kwa akili ya mwanadamu.
Ukweli mmoja kama huo ni ule wa msamaha – hiki ni kikwazo kikubwa! Njia ya kuanza kufanya zoezi hili ni kusamehe vitu vidogo – jaribu kutohukumu – na uendelee kutoka kwa hali ambazo kwa kawaida ungeshikilia.
Kubwa bila shaka ni kujisamehe. Usiwe mgumu sana kwako na utambue wengine wanaweza kukwama katika kujilaumu pia. Anza siku yako kwa haya maneno, “Nimejaa Upendo na Huruma kwangu na kwa wengine.” Endelea kuithibitisha siku nzima.
Hukumu hufanywa kila wakati kuhusu watu na hali. Hilo haliwezi kusaidiwa kwani ni hali ya kibinadamu. Lakini ujanja ni kutoshikilia hukumu hasi, kusonga mbele, kutoa Huruma na Msamaha.
1 Januari 2023
Hapa ni Mabwana wa Mwanga tukiwa na Ujumbe kwako, wakati Mwaka Mpya unaanza.
Tunafahamu sana matakwa ya Watahajudi wote wa Ulimwengu, na wengine kwa kuwepo Amani. Pia kwamba viongozi wa Ulimwengu wangekuwa na maadili ya Kiroho. Hata hivyo, hii lazima itoke kwa umati unaojitolea wa Nafsi nzuri kote Ulimwenguni, zikijaribu bila kuchoka kuleta Mapinduzi ya Kiroho.
Idadi isiyo na kifani ya watu ‘Wanaoamka’ ni ushuhuda wa Kazi nzuri ambayo imefanywa hadi sasa.
Kila siku endeleeni kutuma Upendo na Mwanga kwenye maeneo yenye vita, maeneo ya maafa na kwa watu wanaonyanyaswa au kukandamizwa. Pia, bila kusahau familia yako na marafiki ambao watafaidika sana.
Kamwe usidharau Nguvu ya kutuma Upendo, na sio tu wakati wa Kutahajudi, lakini kwa watu unaokutana nao unapoendelea na shughuli zako za kila siku. Kuwa macho unapoona mtu ana huzuni au mgonjwa, mtumie Nishati yako ya Upendo ili kusaidia kuwainua. Haigharimu chochote.
Acha Upendo utiririke kwa uhuru Ulimwenguni kote – kuondoa chuki, machafuko na kuleta AMANI.
10 Oktoba 2022
Hapa ni Mabwana wa Mwanga.
Kwa kujibu swali lako, yote yanahusiana na kile kinachohitajika kwa wakati huo. Viumbe katika Ngazi za Juu daima Wanatafuta watu wanaofaa ili kutoa Maarifa yao.
Wakati mwingine ni muhimu kuleta habari kuhusu teknolojia mpya. Watu wanatafuta kwa umakini kupata sababu ya maisha yao kitu ambacho dini haitoi.
Inahitaji bidii na kujitolea Kuelekeza ”ku Channel”, lazima uache imani na mawazo yako na kusikiliza kwa ukweli kile kinachosemwa. Mafundisho na maandiko yote yalikuwa muhimu kwa nyakati fulani ili kuleta utambuzi na mwanga kwa watu na kuwasaidia kuelewa nafasi yao katika Ulimwengu.
Kwa sababu ya wakati muhimu katika Mageuzi na maendeleo ya Dunia imekuwa muhimu kutafuta watu wengi wa Kuelekeza Maneno yetu ya kutia moyo, msaada na mwongozo. Kazi yenu imekuwa ya thamani sana kwa ajili hiyo. Mmekuwa muhimu, pamoja na Vikundi vingine vya Kutahajudi, kuwaleta watu kutoka kote ulimwenguni kwenye Uelewa wa kina wa Mambo ya Kiroho, kuwasaidia kuwa na Upendo, Amani na Utulivu maishani mwao.
23 Machi 2022
Unauliza kuhusu Viumbe wengine ambao hawaishi Duniani yaani “Aliens”. Je, dhana yao kuhusu Mungu ni ipi? Wazo lao au konsepti yao ya Enlightenment au Ukombozi wa Ufahamu ni nini?
Yote yanahusiana na “Dimensions”. Aina yoyote ya kiumbe ambayo ingetembelea Dunia, kwa mfano, ingetoka kwenye “Dimensions” za (Juu) – zilizo za juu zaidi kuliko Sayari ya Dunia.
Ni viumbe wa 3D (3 “Dimensions” ) pekee wanaotafuta Umoja ambao haupo – wanaweza tu “kuona” utengano. “Dimensions” zingine zote zaidi ya 3D (3 “Dimensions” ) wapo Viumbe ambao wameunganishwa kabisa – kwa hivyo hakuna haja ya kuwa na dhana hiyo.
Watu duniani walikuwa hivyo, lakini wamepoteza Ufahamu huo – utakuja tena!
21 Machi 2022
Kutoka kwa Mabwana wa Mwanga.
Wakati dikteta anapotuma wanajeshi wake vitani ana matumaini kwamba baada ya muda nchi nyingine zitakata tamaa na kukosa hisia kuhusu mzozo huo – ndivyo inavyotokea. Watu wanaweza tu kuzingatia kwa muda mfupi masuala, hata yale yenye uharibifu mkubwa.
Ni jambo baya sana linalotokea, lakini vita vimekuwa vikiendelea kwa maelfu ya miaka. Ni kwamba sasa vita viko karibu na nyumbani. Kuna ajenda nyingi zinazozunguka kile kinachotokea na hakuna kitu kilivyo kama kinavyoonekana.
Kitu kimoja mnachoweza kufanya ni kutuma Upendo na Huruma kila siku, sio tu kwa Ukrainia bali Ulimwengu mzima – kujaribu kuinua ufahamu wake kutoka ngazi ya chini. Hili likifanywa kwa umakini na Watahajudi wote Duniani kote kwa pamoja, mengi yanaweza kufanikiwa na yanafanikiwa hivi sasa!
Endeleeni kufanya hivyo, kwani kwa kila mmoja wenu kutuma Mwanga na Upendo kwa nia ya kweli kunaleta mabadiliko. Kwa sababu ya matukio ya hivi karibuni watu wengi zaidi wanajiunga kufanya hivi. Fanyeni wote kwa pamoja na mtaona Nguvu halisi ya Upendo.
16 Februari 2022
Hapa ni Mabwana wa Mwanga.
Imesemwa mara nyingi Asili ya vitu vyote ni ya mzunguko, ikimaanisha kuwa kuna vipindi vya wakati kwa matukio yote ya Kidunia na Kosmolojia.
Miaka saba iliyopita ya “Nishati ya WimbiMwanga (Light Wave)” imewapa watu wengi maana ya kweli ya maisha yao. Watu wengi wameamka Kiroho wakati huu pia wameongozwa kufanya Viunganisho vya kuponya Dunia. Kuzungumza kwa lugha ya Kiesoteria, Asili ya mzunguko ambayo inatawala vitu vyote, huja katika seti za saba.
Huu ni wakati mzuri, kwa viwango na ngazi zote, ambao unashuhudiwa hivi sasa na katika miezi ijayo!
22 Desemba 2021
Hapa ni Mabwana wa Mwanga.
Wakati wa mwaka umefika tena kwa watu kutafakari yale waliyoyapata na kujifunza.
Ni muhimu kukumbuka kuwa maisha ni ya mpito. Wale kati yenu mnaofanya mazoezi ya Kutahajudi mara kwa mara mtaweza zaidi kupata uwezo wa kupambana na heka heka za kuwa na mwili wa kimwili.
Maisha ni yanahusu kujifunza “kuachia” hasa wakati huu wa kutokuwa na uhakika. Sio kazi rahisi!
Kwa wale ambao mnakaribia kuanza Safari yenu ya Kiroho ni wakati wa kipekee sana. Tuna furaha kwamba wengi wenu mtakuwa mkipokea Zawadi Maalum ya Kuanzishwa pamoja. Sikiliza kwa makini kile Mwalimu wako anachosema kuhusu unachohitaji kufanya. Kuwa mnyenyekevu na ukubali. Ruhusu Utu na Kuwa kwako kwote kujazwe na Mwanga na Upendo kila wakati unapotahajudi.
Ni kwa kuruhusu Mwanga kutiririka ndani yako ndipo Mafumbo ya Uzima yatafunuliwa. Hatimaye Utatambua Asili yako ya Kweli ya Kimungu.
Kumbuka, Sisi, Uongozi wa Kiroho tuko kila wakati kukusaidia na kukuongoza. Omba kwa unyenyekevu mwongozo wowote unaohitaji. Mara tu unapofunikwa na Mwanga wa Kuanzishwa, utagundua Furaha na Amani ambayo itakuwa nawe kila wakati.
12 Novemba 2021
Unauliza juu ya fahamu.
Hili ni swali zuri sana. Yote yanahusiana na jinsi wanadamu wanavyohusiana na mazingira yao. Watu wengine wangeishi maisha yao kisilika na wanachofahamu ni seti ya mifumo ambayo wanaitegemea kuishi. Unaweza kusema kwamba wanatawaliwa nazo na wangehisi kutokuwa na faraja ikiwa watapingwa, wako “salama” ndani ya mipaka yao.
Kuna wengine, hata hivyo, ambao wana changamoto, na mipaka ambayo jamii inawawekea na “kutoka” kwenye ukungu. Wana mawazo yao wenyewe ya jinsi wanavyopaswa kuishi maisha yao na hivyo ufahamu wao unapanuka ipasavyo. Hii ni picha rahisi sana ya suala gumu sana. Kila mtu ni kiumbe ambaye huongeza ufahamu wake kwa njia tofauti, lakini inasaidia kuelewa aina ya binadamu kama wale wanaokubali hali ilivyo na wale ambao hawakubali.
Sasa tumefikia sehemu ya kuvutia…….
Katika mazoezi ya Kutatahajudi inawezekana Kuwa na Fahamu bila kuwa na ufahamu wa uchochezi wa nje. Hii hutokea wakati mtu anakuwa mmoja na kile anachotahajudi nacho.
Ni dhana ngumu kwa mtu yeyote kuelewa ikiwa hajapitia hii. Inawezekanaje kuwa na ufahamu kabisa, na bado hakuna kitu cha kufahamu!
Lakini watu zaidi na zaidi Wanapitia haya nje ya Tatahajudi. Kila inapotokea Ufahamu wao hupanuka Kiroho na Maarifa yao ya Ulimwengu wa Juu huongezeka. Ni kama kuvunja pazia ambalo hawakujua kuwa lipo.
Hii inaweza kutokea kwa mtu yeyote wakati wowote, hata kwa watu ambao kwa kawaida hawana nia ya kuondolewa katika eneo lao la faraja. Inatia moyo sana na inaweza kubadilisha maisha – na kimiujiza watu wanaweza kuona Ulimwengu kwa njia tofauti kabisa na wakataka kuchunguza Maarifa haya mapya.
Maisha duniani yana uwezekano usio na kikomo. Ufahamu wa mtu unaweza kupanuka Kiroho hadi Upanuzi wa Mwisho, wakati inawezekana Kutambua kwamba kuna Ufahamu mmoja tu – Wao!
7 Septemba 2021
Kutoka kwa Mabwana wa Mwanga:
Miaka michache iliyopita Tuliwaomba idadi ya vikundi vya Kutahajudi kwenye Mwanga na Sauti kufanya kazi ili Kuanzisha idadi ya watu 75,000, kwa pamoja. Hii ndiyo idadi iliyohitajika kufikia kile kinachoweza kuitwa Mapinduzi ya Kiroho!Fikiria kwamba kila mmoja wa hao Walioanzishwa alikuwa Mwanga unaon’gaa.
Haisikiki kuwa kubwa sana, ukizingatia kuwa idadi ya watu Duniani inakaribia bilioni 8; lakini Mwangaza huo nzuri kutoka kwa Watu Walioanzishwa ulitosha kuwaongoza wengine katika kugundua maana ya Juu ya maisha yao.
Tangu idadi hiyo kufikiwa, maelfu ya watu wanapata Mwamko wa Kiroho duniani kote. Athari nzuri imekuwa kwamba watu wengi zaidi wanakubali kuwepo kwa Ngazi zingine za juu za maumbile na mahitaji ya kuchunguza Ngazi au “Dimension” hizi.
Watoto na vijana hasa wana uelewa wa kina zaidi wa Ulimwengu unaowazunguka na wanahoji na kudadisi imani na mafundisho ya kidini ambayo yamekuwepo kwa muda mrefu.
Kwa maneno mengine, watu wa rika zote wanajitenga na hofu ya kuweza kusema kuhusu jinsi Uamsho wao wa Kiroho umebadili mtazamo wao wa maisha na kifo. Labda wanaelewa zaidi asili ya Kuwepo na jukumu lao ndani yake.
Kwa sababu watu wengi wanafuata na ku”tune” kwenye Nishati za Kiroho kwa pamoja, uwezo wao wa kusikia Mtiririko wa Sauti ya Kiroho na kuona Mwanga wa Kiroho umeimarishwa sana. Watu wanaotatahajudi vizuri na kwa kusudi watakuwa na Uzoefu wa kina zaidi, ambao, kwa upande wake, utashusha Maarifa ambayo huchuja katika Ufahamu wa watu.
Kwa hivyo, kwa muhtasari, kuna watu wengi ulimwenguni kote ambao sasa wanafanya Tatahajudi. Kwa wale watu wanaoonewa, wanaohisi kuwa uhuru wao umechukuliwa, basi fanyeni Tatahajudi ili kupata Uhuru wa ndani, Furaha na Amani ambayo tahajudi italeta.
Tafuta Upendo wa Mwisho ndani yenu na uonyesheni kwa familia zenu, marafiki na majirani kila siku.
Ni Upendo pekee unaoweza Kuponya kweli.Ni Upendo pekee unaoweza kuleta Amani ya kweli.
Upendo wa Milele ulio ndani ya kila mtu unaanza kung’aa.
20 Mei 2021
Tunaelewa kuwa watu wanapambana sasa, zaidi kuliko kawaida. Hii ni kwa sababu ya machafuko makubwa yanayoathiri Sayari yenu. Watu hawajui ni nini kitatokea kwao.
Kwa kweli, hii yote ni muhimu ili kufanya mabadiliko makubwa yanayohitajika kwa ajili ya tabia ya kupenda mali na kujithamini. Mungu sio kipaumbele tena katika maisha ya watu na kwa sababu wamemwacha “Yeye” kila kitu kimezidishwa zaidi.
Tuwakumbushe kwa upole watu ambao Wameanzishwa kuwa, ikiwezekana, wasipuuze na kuacha Tahajudi zao ambazo zitakuwa chanzo cha faraja kwao ikiwa watafanya kwa moyo na akili safi. Kwa kweli, wakati wa dhiki na mafadhaiko, huu ndio wakati wa Kutahajudi zaidi, sio kidogo!
Watu wengi wanapata Uamsho kwa upana na wataendelea kufanya hivyo. Ulimwengu na Hali ya Kiroho unabadilika – tafadhali yakubalini mabadiliko haya, vinginevyo maisha yenu yatakuwa magumu zaidi. Tafadhali msishikilie mambo ya zamani, hilo ndilo tatizo kwa watu wengi siku hizi – kumbatieni siku zijazo.
Kuweni na uaminifu kwamba mambo yatakuwa mazuri. Tafadhali msiwahukumu wengine kwa imani na matendo yao, wana sababu zao.
Zaidi ya hapo tunahitaji Upendo kutawala kila tendo. Weka uaminifu wako kwa Mungu na yote yatakuwa sawa.
29 Januari 2021
Kutoka kwa Mabwana wa Mwanga:
Wakati unapojaribu kukubaliana na maafa na majanga yoyote au bahati mbaya, njia ya kushinda ni kusamehe, kubali na jaribu ikiwa unaweza kuona kinachotokea kutoka kwa mtazamo mpana……ingawa ni rahisi kusema hivyo kuliko kufanya!
Wakati kweli unapoelewa na kukubali kuwa kila kitu kina sababu ya kutokea au kufanyika, basi unaweza kuanza kugundua hali halisi ya uwepo au kuwa.
Matukio makubwa – kama yale yanayotokea hivi sasa, yanakuja tu wakati binadamu wanahitaji kujifunza vitu maalum sana.
Tumeelezea hapo awali jinsi watu wanavyopaswa kuwa na upendo zaidi na kutoa, kupunguza kupenda mali na ubinafsi. Ni mabadiliko makubwa na imechukua janga kubwa kuuleta Ulimwengu katika fahamu zake na kuuamsha.
Tunafurahi kusema kwamba mambo sasa yanaenda kwenye mwelekeo mzuri. Wakati ambapo watu wataweza kuonana tena na kutembea kwa uhuru, watachukua hatua tofauti na kuwa tayari zaidi kukubali hali ya Kiroho katika maisha yao.
Daima kutakuwa na wale wanaotamani madaraka na kupata pesa.
Kilichofanyika katika mwaka jana au au zaidi ni kujaribu kuleta mabadiliko mazuri na kuwaonyesha watu kuwa maisha yanaweza kuwa ya urahisi zaidi; kuwa na shukrani kwa kile walichonacho tayari bila kutaka zaidi.
Kupata furaha katika upendo na huduma kwa wengine.
16 Desemba 2020
Hapa ni Mabwana wa Mwanga.
Daima ni vizuri kuangalia Picha Kubwa, kwani inafanya mambo yawe rahisi sana kuelewa.
Mifumo ya Tabia
Tungependa kuzungumza juu ya hii, kwani vitu vyote vilivyo hai vina njia ambavyo zinafanya kazi. Lakini wanadamu wana uwezo wa kubadilisha mifumo yao, kwa mfano njia wanavyofikiria, kuhisi na kuishi. Wanaweza kufanya uchaguzi badala ya kufanya kazi kwa kiasili na kwa silika. Kwa sababu ya hii, si lazima kwenda pamoja na kundi, lakini wanaweza kuwa na njia tofauti.
Kwa hivyo, wanapowasilishwa na mtafutano wa jitihada ya Kiroho, wanadamu wana uwezo wa kufanya maamuzi kulingana na imani na mtindo wao wa maisha. Wakati mtu anaishi Duniani na mambo yao ni magumu, inaeleweka wangependa kubadilisha, ili kutoka katika hali waliyonayo.
Lakini hilo sio jibu! Yote ni kuhusu ridhaa au kukubalika – kukubali wewe ni nani na maisha unayoongoza. Yote yako hapo kukufundisha kile unachohitaji kujifunza. Wakati umejifunza somo fulani, mambo yatabadilika.
Ingawa inaweza kuwa vigumu kuelewa, haswa kwa jinsi mambo yalivyo sasa hivi, kuna Viumbe wengi (Nafsi) ambao wanataka kuchukua miili Duniani kwa sababu, kutoka Ulimwengu wa Mbinguni Tunaona vitu kutoka kwa mtazamo tofauti sana.
Wakati uliotumika Duniani ni Zawadi ya kutumiwa kwa busara na kwa shukrani.
19 Novemba 2020
Hapa ni Mabwana wa Mwanga.
Hamu ya taarifa na habari toka kwenye vyombo vya habari haijawahi kuwa kubwa zaidi kama ilivyo sasa. Kwa ujumla watu wana muda zaidi wa kuangalia hadithi na habari ambazo zinaathiri sana uhuru wao na jinsi wanayoishi. Ni kama sumaku – huwavuta watu ndani. Huu ni wakati mgumu sana kwa watu wengi kila mahali. Wanaogopa nini kitatokea siku zijazo.
Shida huibuka wakati watu wanapotumia muda mwingi kupindukia kwa mtiririko wa habari zisizo na mwisho.
Hii inapaswa kuachwa. Tunahitaji kukuambia kuwa kutakuwa na hadithi zaidi na zaidi na nakala zinazokuja, zinazohusiana na Viongozi wa Ulimwengu, Siasa, Dini na Afya. Lakini hauhitaji kuwa na wasiwasi, kwa sababu, kama kawaida, mambo yanaweza kujisawazisha yenyewe.
Zawadi kubwa zaidi ambayo unaweza kuupatia Ulimwengu sasa ni kuwepo kikamilifu katika Tahajudi zako na ikiwezekana ongeza muda unaotahajudi. Jizamisheni tu katika Nishati tunayotuma na kuwa watulivu na kutulia. Hii italeta amani kwa akili zenye matatizo na uelewa zaidi kwa Nafsi.
Oktoba 5, 2020
Hapa ni Mabwana wa Mwanga.
Tumekuja kuzungumza na wewe juu ya jinsi ya kuishi katika Ulimwengu wa misukosuko, ambapo hakuna jambo linaonekana la maana tena.Jambo la kwanza kukumbuka kila wakati ni kwamba watu wana uwezo wa kubagua – kujifanyia na kujua wenyewe sababu zinazosababisha kwa ujumla hali ya ulimwengu kwa sasa. Daima angalia kwa mtazamo Mkubwa na uone kuwa maisha Duniani daima yamekuwa na changamoto zake.
Tumeelezea hapo awali kuwa kusudi la maisha ni kupenda na kujifunza, ni jukwaa bora zaidi la kufanya hivi!
Unapokabiliwa na changamoto, kila mara jaribu pia kuangalia ndani ili upate majibu. Njia bora ya kufanya hivyo, kweli ni, Kutahajudi. Jaribu kukaa chini na “picha tupu” – usilete maoni yoyote yaliyotungwa katika Kutahajudi kwako.
Uliza maswali ya kutoka moyoni na utapokea majibu ambayo yana maana kwako. Labda sio mara moja lakini kadri wakati unavyopita unaweza kupata maoni yakichujika na kuingia kwenye ufahamu wako.
Upendo ambao utapata katika Kutahajudi kwako utakupa faraja kupitia hali yoyote. Kuendelea na mazoezi kunaweza kukupeleka kwenye Lengo la Mwisho la Mwanadamu – Chanzo cha Uumbaji, Jibu la mwisho!
Julai 3, 2020
Hapa ni Mabwana wa Mwanga.
Tunafurahi kukuambia kwamba idadi ya watu waliopata Initiation (Walioanzishwa) Duniani imezidi hata lengo lililowekwa. Sasa tunaenda kwenye awamu mpya!
Tulikuambia kuwa kuna vikundi vingi ambavyo huanzisha watu kwenye Mwanga na Sauti. Siku hizi, kwa kweli, wengi wanapata Uamsho kwa hivyo hii imeongeza idadi.
Mambo yanabadilika ghafla, kama unavyojua, kwa sababu ya hali iliyopo Duniani sasa. Hii imeleta idadi kubwa ya watu kutahajudi.
Mei 28, 2020
Hii ni kutoka kwa Mabwana wa Mwanga
Wakati Kiumbe anapochukuwa mwili, unajua kuwa ni kwa kusudi fulani, maisha ya kuishi kulingana na ‘mpango’ ambao tayari ni thabiti. Hakika, kuna kuchepuka kutoka kwenye mpango huo ambao unaweza kuanzishwa wakati fulani kwenye maisha. Lakini kisichojulikana kwa ujumla ni kuwa kusudi linaweza kubadilika kukiwa na mazingira fulani.
Katika nyakati hizi ambazo siyo za kawaida ambapo kuna machafuko mengi hapa Duniani, inakuwa muhimu kuwa na mwelekeo kwenye mambo ya Kiroho.
Kwa hivyo, watu wengi ambao wangekuwa hawajachukuwa miili kwa ajili ya kuwa na maisha ya Kiroho, hujikuta wanakuwa na msukumo na kuwa na hamu kubwa ya kupata maana halisi ya maisha kupitia Tahajudi.
Watoto wengi waliozaliwa nyakati hizi wana kusudi moja kubwa la kueleta Nguvu Imara ya Kiroho.
Mei 10, 2020
Hapa ni Mabwana wa Mwanga wanakuja kuzungumza na wewe kuhusu virusi ambavyo bado vinaathiri sehemu nyingi za Duniani kwa wakati huu.
Tunajua kuwa watu wengi wanateseka kwa sababu hiyo, na hawana uhakika juu ya maisha yao ambayo kwa namna fulani yamechukuliwa kutoka kwao.
Tafadhali aminini kuwa ingawa mambo yanaonekana kuwa yanaenda mrama, yatapita. Mtaangalia nyuma na kugundua kuwa wakati huu kulikuwa kunahitajika mabadiliko ili Dunia iweze kukua Kiroho – kwa watu binafsi wawe na ufahamu mkubwa juu ya uhifadhi na uimarishaji wa Dunia.
Tunatumai kwamba, wakati huu wa kutengwa na upweke, watu watafikiria sana jinsi wanavyoongoza maisha yao na watatekeleza mabadiliko yoyote yale kwa faida yao wenyewe na wanadamu.
March 31, 2020
Hii ni kutoka kwa Mabwana wa Mwanga.
Kwa hakika ni wakati sasa kwa Watahajudi wote Duniani kuungana pamoja kwa kusudi la pamoja la kuleta Mwanga na Upendo kusaidia kwa ajili ya woga na kutokuwa na hakika kuhusu virusi.
Watu sasa wana wakati zaidi wa kutafakari kuhusu maisha yao. Kama tulivyosema mara nyingi, maisha nia yake ni Upendo na Utoaji, na hii ni fursa nzuri ya kuongeza muda ambao wanatahajudi, ili kuwasaidia binadamu wenzao.
Watu wengi, sana sasa wanateseka aidha moja kwa moja au kwa namna nyingine kwa sababu ya virusi. Wengine wanafanya kazi kweli kwa bidii, huku wanahatarisha maisha yao.
Sasa ni wakati wa kuleta Mwanga na Upendo kwenye sayari kuliko ambavyo kamwe haijawahi kutokea.
Tunatumaini kuwa binadamu sasa wako tayari kusimamisha kasi ya maisha na kutafuta na kupata Upendo zaidi, Furaha na Amani.
9 Januari 2020
Huu ni ujumbe kutoka kwa Mabwana wa Mwanga kuashiria mwanzo wa muongo (decade) mpya.
Mtakuwa mkishuhudia majanga yanayoendelea ulimwenguni kote na labda mnashangaa jinsi itakavyowezekana kuyakwepa na kuishi, na jinsi ya kufanya mambo kuwa bora.
Tafadhali eleweni kuwa pamoja na ukatili wote ambao mnaosikia wakati wote kuna kazi kubwa na ya kushangaza inayofanywa na Wafanyakazi wa Mwanga na sio kutoka kwenye sayari hii tu lakini wasaidizi kutoka kwa ulimwengu zilizoko mbali. Kila moja kwa njia zao tofauti wanashiriki kwa namna yao.
Kundi la Watahajudi wa Lightwave wamepewa kazi yao ya kufanya taswira ya kupeleka Upendo, Mwanga na Utulivu kwa roho zote ambazo zimejaa chuki na hasira. Jaribuni kufanya hivi vizuri zaidi kama mnavyoweza, kuweka taswira hii kwenye akili zenu kwa dakika chache kila siku wakati mnatahajudi.
Upendo na Mwanga mnaotuma unapaswa kushinda ikiwa watu wa kutosha wakifanya kazi hii muhimu sana.
12 Novemba 2019
Kutoka kwa Mabwana wa Mwanga
Inaonekana dhahiri kwamba watu sasa wanaweza kuongea na kufurahia kuwaambia wengine juu ya Uzoefu wao wa Kiroho. Ni kwa kufanya hivyo kwamba wanaweza kusaidiwa kuchunguza kwa undani zaidi upande wa Kiroho wa maumbile yao. Ni muhimu sana kuwasiliana na kuelezea kile walichogundua ili kuwahamasisha na kuwatia moyo wengine kufanya vivyo hivyo.
Huu ni mwanzo wa awamu mpya, wakati watu wanakuwa na uzoefu huu bila kutegemea. Ni kana kwamba mtazamo wao unabadilika na kufahamu zaidi mambo ya Kiroho badala ya ubinafsi wao mdogo.
Kadri tunavyoendelea kusonga mbele ni muhimu pia kukumbuka kutafuta mema ambayo yanatokea kote Ulimwenguni. Wakati mwingine, wakati mambo yanapoonekana kuwa mabaya ni vigumu kupata raha za maisha. Saidianeni kila wakati kwa maneno ya fadhila au kutuma Mwanga na Upendo.
Maisha hutoa changamoto nyingi. Yafikirie maisha kama shule ya kufundishia masomo.
Punde tu funzo au somo linapoeleweka ndivyo ambavyo haraka zaidi mtu anaweza kuendelea mbele na kuimarika.
31 Octoba 2019
Sisi, Mabwana wa Mwanga tunataka kukupa ujumbe.
Inawahusu watu wote wanaotahajudi na haswa wale wanaotahajudi kwenye Mwanga na Sauti.
Kadri watu zaidi na zaidi wanavyoamka bila kutegemea na wanawasiliana na Nguvu za Mwanga na Sauti Tunafahamu uongezekaji wa Mwanga wa Kiroho kwenye Sayari yote. Mnapotahajudi kwa vikundi basi Mwanga ni mkali zaidi na wazi, kwa hivyo ina athari nzuri na kubwa, ikiondoa giza ambalo linaenea na kufunika maeneo mengi ya Dunia.
Kadiri mnavyoweza kuzingatia na kuwa na kusudi la kuifanya dunia kuwa mahali bora, basi itafanyika. Ni Azimio na Mapenzi Yenu kwa pamoja ambayo hufanya tofauti. Inatengeneza ongezeko la Nguvu inayoenea kila mahali.
Tulisema hapo awali, kwamba hamtabui Nguvu ambayo iko kati ya watahajudi. Ikitumika kwa pamoja kama nguvu ya wema inaweza kuleta tofauti kubwa.
Kuwasaidia wengine kwa Mwanga wako kutakusaidia wewe pia. Kadri unavyotoa Mwanga zaidi, ndivyo unavyozidi kupata na kurudishiwa Mwanga zaidi. Inafanya kazi kwa njia hiyo.
1 Octoba 2019
Ni fursa kubwa kwangu kukuandikia ujumbe huu kutoka kwa Uongozi wa Kiroho.
Sisi, katika Ulimwengu wa Kiroho tumeunganishwa na wewe wakati huu maalum sana.
Kuwa na wengi wenu kiasi hiki Walioanzishwa pamoja katika eneo lenye baraka kweli ni hatua kubwa katika Uamsho wa Kiroho wa Sayari ya Dunia. Yaani, Dunia kama Kiumbe na wakazi wake wote.
Hasa Tumevutiwa sana na Upendo na Furaha inayopatikana kutoka kwenye mioyo yenu kwenda kwa kila mmoja wenu na kwa ulimwengu kwa jumla.
Bado kuna maeneo mengi ambapo kuna vita, njaa na magonjwa. Tungependa kuwaomba nyinyi wote kuzingatia kupeleka Upendo wenu kwa umoja katika maeneo haya, kujaribu kufuta migogoro, kuponya wagonjwa na kulisha wanaokufa na njaa.
Kadri watu zaidi na zaidi wanahisi mwito wa Uamsho wa Kiroho, Upendo na Mwanga utashinda Giza kwenye Maeneo haya.
Maelfu ya watu mnapotahajudi kwa pamoja, kweli mtaleta mabadiliko.
Kila kitu kimeunganishwa na Nguvu ya Mwanga itaangaza na kuchomoza.
24 Septemba 2019
Hii ni kutoka kwa Mabwana wa Mwanga
Kuwa na imani kwako mwenyewe. Hii ni muhimu kwa sababu, wakati Ascension inakaribia lazima utambue kuwa hakuna mtu yeyote muhimu zaidi kuliko mtu mwingine. Kila mtu ana sababu yao ya kuwa Duniani kwa wakati huu, kama ilivyo pia kwa kila kiumbe.
Hakuna kitendo ambacho ni muhimu zaidi kuliko kingine, hii ni ngumu kuelewa, kwa sababu ili kuona kwamba ni kweli lazima utoke nje ya Ulimwengu utazame nyuma. Kila kiumbe kina kazi yake maalum au jinsi ya kuwa.
Kwa hivyo, unapoamka asubuhi, fikiria siku yako kuwa imejaa Upendo, Kupenda na Kujifunza. Usiku, unapofikiria juu ya siku nzima, jiulize, kwa ujumla, unafurahi jinsi siku ilivyokwenda. Ikiwa sivyo, kwanini?
Kinachofanya siku nzuri kwa mtu mmoja ni tofauti na mtu mwingine. Watu wengine wanahitaji kujaza wakati wao na vitendo; wengine wana nafasi za kutafakari, kuchukua muda na kupumzika. Unaunda ukweli wako mwenyewe.
Suala zima ni kuwa na Kiasi na Uwiano, kama Tulivyosema hapo awali
17 Septemba 2019
Hii ni kutoka kwa Mabwana wa Mwanga kuhusu Kutoa
Hakuna chochote Duniani ambacho kwa kweli ‘ni cha’ mtu yeyote. Hiyo inamaanisha ingawa kutoka katika umri mdogo sana watu hufundishwa kuwa hiki, au kile ni chako sivyo ilivyo.
Wewe unakopa tu au unakopeshwa tu vitu kwa wakati uponaishi hapa Duniani. Hii inaweza kuwa dhana ngumu kuelewa lakini ni dhana ambayo ni muhimu sana kuelewa.
Wakati watu zaidi na zaidi wanaelewa kuwa hawamiliki kitu chochote basi wanakuwa wakarimu zaidi..
Mara nyingi utaona kuwa watu wakarimu sana ndio ambao wanacho kidogo zaidi cha kutoa. Hii inaweza kuonekana kuwa kitu cha ajabu na kushangaza hadi utakapogundua kuwa watu hawa mara nyingi ndio wenye furaha zaidi. Watu wenye furaha kwa ujumla ni wakarimu zaidi.
Kuwa na utajiri mkubwa kwa kweli huleta majukumu yake yenyewe, kujitahidi kutunza utajiri huo kunaweza kusababisha wasiwasi na baadaye magonjwa.
Kadiri unapojaribu zaidi kushikilia kitu, ndivyo unavyohisi unakiachia na unakipoteza.
Uwiano na kuwa na Kiasi ndio ufunguo.
7 Septemba 2019
Huu ni ujumbe kutoka kwa Mabwana wa Mwanga kwa wote wanaotafuta Hali ya Kiroho, kwa wale ambao wamepokea Mwanga na Sauti na wale ambao wamepata Enlightenment.
Wakati watu wanapoanza kuelewa kuwa kuna kusudi kubwa la maisha kuliko kuishi tu, maisha yao hubadilika kwa kuangalia karibu yao na kuona, labda kwa mara ya kwanza, kwamba kuna uzuri katika mazingira yao ambao walikuwa hawajauona kabisa.
Daima kuna uzuri unapatikana ikiwa mtu anaangalia kwa nguvu za kutosha. Inaweza kuwa ua, au mti, au mtu anayesema ‘habari’ ambaye kwa kawaida alikuwa kama hakutambui.
Mara tu mtu, au kikundi cha watu wanapoanza kugundua uzuri katika vitu, au watu, basi jambo la kushangaza ni kwamba uzuri huanza kukua katika hali isiyo ya kawaida. Ghafla maisha yao hubadilika kutoka kwa uwepo wa kipekee sana na wa tamaa za kibinafsi hadi kukubalika kwa kila kitu na vitu vyote, kama vilivyo, bila kuhukumu.
Hii kawaida inaweza kuchukua miaka mingi, lakini sio lazima ichukue muda mrefu.
Wakati mtu anatembea katika Njia ya kuelekea kwenye Enlightenment, inawezekana kubadilika haraka sana, kwa sababu unagundua kuwa unapohukumu kitu chochote, unajihukumu mwenyewe.
Wakati uzuri wa ndani unapogundulika na kweli kutambulika, basi uzuri wa nje hugundulika pia.Fikiria ni Uhuru kiasi gani unaopatikana. Kweli Uzuri uko kwenye jicho la mtazamaji.
1 Agosti 2019
Hii ni kutoka kwa Mabwana wa Mwanga, kujibu swali lako toka moyoni.
Sisi katika Ngazi za Kiroho tunaangalia wakati wote na hakuna kitu kinachotokea au kupita bila kutambulika, kama tulivyosema hapo awali.Tangu mwanzoni wakati Mwanadamu alipomtafuta Muumba wake, imekuwa utafutaji wa ndani wa kiroho, kwa nia safi. (mara nyingi ikitanguliwa na mtikisiko wa ndani wa maisha na maumivu, ya kimwili au vinginevyo)
Utafutaji huo wa ndani, mwishowe, ghafla bila kutarajia ulimwonyesha mtafutaji wa Ukweli Chanzo chake – Umoja wa Vitu vyote. Hii ilikuwa nadra sana.
Kadri muda ulivyoendelea, mambo yalibadilika na mchakato wa Uanzishwaji (Initiation) ukaanza – kufanya mambo yaendelee Kiroho – kuwaongoza watu kwa “kuwaonyesha Mwanga” na kuwaongoza kwenye Safari ya Kiroho, ambapo ndipo tulipo sasa.
Katika siku zijazo, Tungependa kuona kuwa kadiri watu wanavyoendelea kukua na kubadilika kuwa Viumbe wa Juu, wakati ‟Ascension” inavyokomaa, watu watarudi kwenye Kujitafuta wenyewe, lakini kwa uelewa wa ndani zaidi wa “Roho” na mahali na wajibu wao kama Binadamu . (kuwa wame‟Evolve” zaidi kabla ya kuanza Kutafuta) Itakuwa aina ya ‟Gnosis” ambayo imepenyeza na kuenea ndani ya Nafsi zao.
Kuna wale ambao tayari hufanya hivi na tunatumaini kwamba wakati Mwanga unapotembea na kuzunguka katika giza la udongo (matter), basi Nafsi zaidi na zaidi ‟zitachukuliwa” na Nguvu hii mara moja bila kutegemea kama zamani. Lakini tofauti itakuwa, ni kawaida na sio nadra.
Hii Tunarahisisha – lakini kwa kweli ni ngumu zaidi.
22 Julai 2019
Hapa ni Mabwana wa Mwanga.
Hakika ni kwamba watu ambao hutahajudi wako tayari zaidi kwa safari yao ya maisha yajayo na zaidi.Kuna sababu nyingi za kuanza Kutahajudi. Watu wengi, wanapoanza, hawatambui ni wapi tahajudi itawapeleka. Wanasikia wengine wakisema kwamba inasaidia kujielewa binafsi na hii ni kweli, lakini hiyo inamaanisha nini?
Baada ya muda wanagundua kuwa sasa wanaweza kuelewa watu wengine, na kwamba kuna uhusiano kati ya kila mtu. Kila kitu kinachotokea kipo pale ili kumwonyesha mtu safari yake ya kibinafsi kwenye maisha, masomo yake na maendeleo yake katika harakati za kuwa kwao Duniani.
Ikiwa mtahajudi ameanzishwa kwenye Njia ya Mwanga na Sauti, kuna fursa ya kushuhudia Mwanga wa Kiroho na Sauti ya Kiroho ambazo zimezungumziwa na Mystics au Waalimu wote wakuu wa Kiroho.
Mtahajudi anachukuliwa katika Ngazi zingine za Maumbile na Ufahamu ambazo watu wengine wanaweza kuelezea kama “Kuchungulia Mbinguni” (“Glimpse of Heaven”) na wengine kama Utambuzi wa kweli wa Kuwa kwao.
Hii ni zaidi ya yote ambayo wangeweza kuota na kufikiria na wakati mwingine wanaona kuwa ni vigumu kuelezea wengine kile walichoona au walichosikia katika “Ulimwengu wa Mbingu”.
Kwa wale ambao wameyeyuka kwa kweli kwenye Muungano wa Mwanga na Sauti na wameguswa na Upendo Kamili na Kukubalika ambako hupatikana kweye Mwanga na Sauti, kamwe hawawezi kuwa na hofu yoyote ya kifo – au ya kupita kwao kwenye Maisha na Uzima baada ya kifo.
9 Juni 2019
Hii inatoka kwa Mabwana wa Mwanga
Inapaswa kueleweka kwamba Kuanzishwa (Initiation) sio kwa kila mtu. Kuna watu wengi ambao hawawezi kuwa na hamu na nia, hata kama wangeelezwa kwa kiasi gani kuhusu faida yake. Sio kitu kinachowagusa.
Halafu kuna wale ambao wanashauku na wanataka kujua zaidi kuhusu Kuanzishwa. Labda wao hawajui jinsi Dunia itakavyokuwa katika kipindi cha miaka 5-10 na inawapa wasiwasi. Au labda wao wanakua wazee na wanashangaa kwamba nini kweli kinachotokea kwao wakati wanapokufa.
Tunachoweza kukwambia kwa hakika ni kwamba kila mtu aliye na kiu ya Maarifa ya Kiroho ya Kweli na ambaye anataka Kuanzishwa (Initiation) atapata majibu ya maswali yake. Pia hisia ya nguvu ya ndani na kuridhika.
Watu watauliza, Kwa nini Mwanga na Sauti, je hakuna njia nyingine za kupata uamsho wa Kiroho? Naam, ndiyo, watu hupata maono mazuri na hisia za Upendo. Lakini tofauti kubwa ni kwamba hawawezi kuonyesha wengine jinsi ya kufanya ili kupata maono haya.
Mwanga na Sauti ni umoja, Nishati yenye wema na kujali, inayompa Mtahajudi njia, ambayo inapofuatwa hadi mwisho wake, inaweza kuwaonyesha Uwazi na Urahisi (Simplicity), Ajabu na Maajabu ya Enlightenment.
Lakini huo ndiyo mwanzo wa kuchunguza uhuru mpya unaopatikana.. Hauna kikomo.
4 Juni 2019
Sisi ni Mabwana wa Mwanga.
Tunahitaji kuzungumza na ninyi juu ya “Ascension” na jinsi itakavyoathiri binadamu.
Mko kwenye ukingo wa kitu cha kushangaza kabisa. Jinsi watu watakavyokabiliana na hili inabakia kuonekana. Kila mmoja wenu ambaye, kwa namna fulani, amekuwa na Uamsho wa Kiroho ataweza kukabiliana na kitakachotokea na kinachotokea hivi sasa.
Mambo yanabadilika haraka hivi sasa, Dunia inabadilika kuzidi ufahamu wa mtu yeyote yule. Itaendelea kwa namna hii kadri teknolojia inavyozidi kuwa ya utata zaidi na zaidi. Watu ambao wameamka Kiroho zaidi wataweza kutoathirika sana na mabadiliko haya.
Watatambua kwamba Dunia ni sehemu ndogo tu ya Ulimwengu mkubwa na kinachotokea ni kwa sababu ya Ulafi, Kugombea Nguvu na Madaraka, Ubinafsi na ukosefu wa Upendo. Wao wataelewa kinachoendelea na watakabiliana vizuri na changamoto hii.
Kinyume itakuwa kweli kwa wale wanaokataa kuona kwamba maisha hayamaanishi kuishi katika “hedonism” na ubinafsi.
Kwa ninyi nyote wafanya kazi wa Mwanga mnaofanya kazi bila kuchoka kujitahidi kuinua ufahamu wa binadamu, tunasema Asante.
16 Aprili 2019
Hii ni kutoka kwa Mabwana wa Mwanga.
Sisi tunafuraha sana kusema kwamba harakati za New Lightwave zinakua haraka sasa. Hii ni kutokana na makundi na watu binafsi wanaojitolea duniani kote ambao hutia moyo wengine kwa furaha na shauku.
Sio idadi tu ya watu ambao wanaanzishwa ambayo sisi tunaangalia, lakini jinsi wanavyojitolea ili kuendelea mbele kwenye Njia.
Watu wanahitaji kuleta chini Nguvu kutoka Ngazi za juu za Kiroho mara kwa mara. Kwa Kutahajudi vizuri, hawatakuwa wanajiinua wenyewe tu Kiroho, lakini pia kuwa nguzo ya Mwanga kwa wengine.
Jinsi ambavyo watu wanakuwa na Ufahamu wa Kiroho Tunaona mabadiliko makubwa yanayofanyika. Itakuwa kana kwamba wanawaamsha wakazi wa Sayari kuona mambo kwa namna mpya. Sio tu kutoka kwa mtazamo wa Kiroho, lakini watakuwa wanaangalia tabia za zamani na mawazo ya kizamani kwa macho mapya.
Hii inahitaji kutokea SASA!
29 Machi 2019
Kutoka kwa Mabwana wa Mwanga – Kila kitu …… kila chembe kwenye Ulimwengu ina Ufahamu au Uelewa wa yenyewe na kila kitu kingine.
Wakati Mwanadamu anakusanya mabilioni ya atomi ambazo zinahitajika kutengeneza mwili, basi atomi hizi huchaguliwa hasa kwa ajili hiyo. Mwamba, au mti, au simba zitakuwa na seti tofauti ya atomi. Fahamu ya jiwe, kwa mfano, ni pungufu.
Uwezekano upo, wa kila binadamu kuwa na uwezo wa kufahamu Nguvu ya Mwanga na Sauti. Hata hivyo, kila mtu ana seti yake mwenyewe na ya kipekee ambayo inaweza kupunguza uwezo wao wa kutahajudi. Binadamu wengi wanazo hisia tano, ambayo ina maana kwamba wanaweza kuzitumia kujijua wako wapi katika dunia hii ya kimwili. Hivyo Uelewa na Ufahamu huo huo unaweza kutumika kutafuta na kupata lengo la Ndani au madhumuni ya Nafsi.
Kadri wewe unavyojua zaidi na zaidi Ulimwengu wa Kiroho na “Intelligence” kubwa inayoshikilia Ulimwengu na zaidi, atomi zako “zinashtushwa” katika maandalizi yako kwa ajili ya Ufunuo zaidi, mpaka kufikia hatua ya mwisho ya safari yako, ile ya mtu aliyekuwa Enlightened.
Hata baada ya hapo unapaswa Kutahajudi kila siku, kwani huachi kujifunza na kamwe huachi kukua Kiroho, hadi kifo chako na baada ya Kifo.
12 Machi 2019
Tunazungumza na wewe kutoka kwenye Ngazi za Kiroho – kundi Letu ambao tunataka kuzungumza na kila mmoja wenu ambaye anataka kuleta mabadiliko Duniani. Tumekuambia mara kwa mara juu ya Nguvu kubwa ya Kiroho ambayo watu wanajikuta wanaipata na kuisikia bila kutegemea. Hii inatokea ili kumwamsha Binadamu ili kuendeleza hali yao ya Kiroho.
Tunajaribu, kwa njia ya ujumbe wetu kuwahamasisha watu kutafuta mwalimu wa Tahajudi ya Mwanga na Sauti na kuanzishwa katika safari yenye msukumo ambayo hawajawahi kamwe kutembea. Inasemekana kuwa mtu mmoja katika kila watu elfu moja ataleta mabadiliko na tofauti katika Dunia. Wengi wako kwenye wasiwasi tu na mahitaji yao wenyewe.
Kwa mwamko wa Kiroho kweli una nafasi ya Kuwa mtu maalum haswa. Utapewa zawadi ya ajabu ambayo, wakati ukifika, wewe pia utaweza kuwapa wengine.
Kila kitu juu ya Dunia ni cha muda mfupi, hakuna kitu kinachokaa au cha kudumu – lakini Nguvu hii haiwezi kuchukuliwa kamwe. Mara inapotolewa basi mtu mpya aliyeanzishwa atakuwa na Hali ya Ufahamu uliyopanuka.
Tafadhali angalialieni kwa uangalifu maandishi haya, yanawaonyesha Hekima ya Wakati mnaoishi sasa. Furahia na kuwa na faraja kwamba pamoja na shida zote ambazo zinaikabili Dunia kuna Nguvu za Ngazi za Juu ambazo unaweza kuzitumia kutahajudi ili kuweza kufahamu kila kitu.
3 Machi 2019
Hapa ni Mabwana wa Mwanga tunazungumzia kuhusu Nafsi (Soul).
Wakati Nafsi inachukua mwili ni kwa kusudi maalumu sana. Hakuna Nafsi inayochukua mwili bila kusudi – kila kitu kimepangwa kabla, mahali ambapo mtu huyo atazaliwa na kwa wazazi gani. Ndugu, jamaa zake na rafiki vyote vimepangwa pia. Kisha mienendo yote inaangaliwa.
Ni muhimu kwa Nafsi kuwa “imesahau” kila kitu kilichotokea kabla ya kuzaliwa hivyo kwamba maisha yanaweza kuiishika bila ya kujua miili ya awali ambayo Nafsi imeshachukua na kwa ajili ya mipango kabla ya kila maisha. Kama vile ambavyo kuna sheria kwenye kila jamii pia kuna sheria za Ujumla (Universal laws). Moja ya sheria ni kwamba kila Nafsi ina nafasi ya kutimiza lengo lake katika kila maisha.
Mara nyingi, wakati mtu anapochukua mwili, hawawezi kufikia lengo hilo. Lakini kwa vyovyote vile, atakuwa na fursa nyingine katika maisha au mtiririko wa maisha ya baadae.
Jinsi maisha yanavyoendelea inabidi iwe wazi zaidi ni kwa nini watu fulani wako karibu nao na ni nini wanahitaji kujifunza. Maisha yote yanahusu Upendo na Kutoa. Hivyo, kama kuna mtu huangalia ndani na kwa kweli kujijali tu wao wenyewe, basi hawawezi kuwa na uwezo wa kuona jinsi matendo yao yanavyoathiri watu wengine. Hii ni njia ya ki‟Ego” ya kuishi ambayo si namna nzuri kwa kusonga mbele kwa ajili ya mabadiliko.
24 Februari 2019
Hii inatoka kwa Mabwana wa Mwanga, wakizungumzia kuhusu Ego
Ego ni moja ya changamoto tano ambazo mwanadamu anahitaji kukabiliana nazo. Zingine zikiwa ni Uzinzi, Hasira, Uchoyo na Kujishikamanisha. Wakati mwingine hujulikana kama Vidole Vitano vya Kifo. Bila Ego mwanadamu hawezi kuishi – inamaanisha ule ubinafsi au “Mimi”.
Lakini, kama ilivyo kwa kila kitu katika maisha inabidi kuwe na usawa. Unahitaji kuzingatia mambo yako na uhakikishe kuwa mahitaji yako ya kidunia na kimwili yanatoshelezwa.
Lakini kutokea pale ambapo tunaangalia Dunia na wakazi wake hivi sasa tunaweza kuona kwamba hisia ya Ego imeenea sana katika maisha ya watu wengi. Tunapaswa kusema kwamba hata watu ambao wanaweza kujihesabu kuwa wa Kiroho wanaweza kuwa wachoyo na wabinafsi.
Hii ina athari mbaya kwenye usawa wa Dunia na inahitaji kushughulikiwa. Wakati Ego ni nje ya usawa huharibu hisia ya amani na ustawi kwa mtu, swala ni kuhakikisha kwamba unatilia maanani umuhimu wa watu wengine. Hiyo ndivyo jamii inavyofanya kazi vizuri na kila mmoja jinsi anavyoweza kuonyesha hali yao ya Kiroho na upendo wa kiasili kwa Dunia.
11 Februari 2019
Kutoka kwa Mabwana wa Mwanga
Hebu sasa tuangalie neno la tatu na la mwisho – Kukubali
Kuna mambo mengi kwa neno hili – kwa ufupi hii ni pamoja na:
Kujikubali mwenyewe – kuwa na furaha na kuridhika na jinsi ulivyo.
Kuwakubali watu wengine, bila kujali jinsi Walivyo.
Kukubali hali, binafsi au vinginevyo.
Jinsi ambavyo mtu Anatahajudi zaidi, anatambua kwamba ingawa inaweza kuonekana kinyume chake, hawawezi kutawala maisha yao. Kwa maneno mengine – kinachotokea, kinatokea ikiwa kimetakiwa kuwa. Watu wanaweza kutamani maisha yao kuwa namna fulani lakini wakati mwingine haiwezekani ikiwa sivyo ilivyopangwa.
Mbinu ni Kukubali mambo ya maisha ambayo hayawezi kubadilishwa na kutambua kwamba kuna sababu ya hali hiyo. Tunajua kuwa hii ni rahisi zaidi kusema kuliko kutenda, hasa katika maeneo ya vita, hali ngumu ya familia, magonjwa ya muda mrefu nk.
Lakini hata hivyo, katika hali nyingi inawezekana kujifunza kutopambana na hali fulani, lakini badala yake kuikubali na kuangalia ni kitu gani ambacho unaweza kujifunza kutoka kwenye hali hiyo.
Binadamu yuko Duniani ili Kupenda na Kujifunza.
8 Februari 2019
Kutoka kwa Mabwana wa Mwanga
Sasa tunakuja kwenye neno la pili …… .Kusamehe
Unaweza kusema kwamba ikiwa Upendo umeonyeshwa kikamilifu, basi msamaha na kukubalika kutaonyeshwa kwa wengine moja kwa moja. Hata hivyo ni muhimu kuyazungumzia tofauti ili kuelewa umuhimu na maana zake kamili.
Watu wanaongea juu ya kusamehe wengine lakini hawawezi, au hawako tayari, kujisamehe wenyewe. Jambo hili ni muhimu sana. Kumsamehe kweli mtu ambaye amekukosea sana kunahitaji kuwa na moyo safi.
Wakati mtu hataki kusamehe, basi mara nyingi sababu ni mbili.
Kwanza, mtu huyo hajatazama ndani yake ili kupata vitu vibaya ambavyo labda ameshawahi kufanya. Pili wanahitaji kutambua hofu ambayo inawazuia kutambua kwamba wao pia wana makosa. Hiyo sio kusema kuwa wao ni watu mbaya, lakini hakuna mtu aliye kamili. Mtu hawezi kusema kuwa amsamehe mtu mpaka awe amejisamehe. Ikiwa hilo linaweza kufanyika basi linasababisha uhuru mkubwa.
3 Februari 2019
Hii inatoka kwa Mabwana wa Mwanga.
Wakati Njia hii mpya ya LightWave “ilipozaliwa”, Tulichagua maneno matatu ambayo watu wanaweza kujiunga na kuhusiana nayo ili kusaidia kutoa Ujumbe Wetu. Yamekuwa msingi wa Mafundisho.
Jinsi Njia inavyokua, Tungependa kurejesha haya maneno na kuyazungumzia kwa undani, kuanzia la kwanza na ambalo ni muhimu zaidi – Upendo.
Haishangazi kuwa neno hili linatumiwa sana. Kwa kawaida hutokea katika aina zote za mawasiliano katika familia, jamii na makundi kwa sababu watu wanataka/wanahitaji kuonyesha upendo kwa kila mmoja. Kwa kweli, ikiwa watu zaidi katika familia, makundi na jumuiya wangeonyesha zaidi Upendo na urafiki kwa kila mmoja ugomvi na kutoelewana kutapungua katika Dunia.
Lakini Upendo huu tunaozungumzia inabidi kuanzia mahali fulani, na kwamba, ni ndani ya mtu binafsi. Ikiwa mtu amekuwa na bahati ya kukua katika jumuiya ambapo watu ni wema na Wanapendana, basi ni rahisi kutoa Upendo. Hata hivyo, Ikiwa kumekuwa na hasira, kutoelewana na chuki wakati wote, Upendo utakuwa wapi ndani ya mtoto? Mbegu inapaswa kusaidiwa na kukuzwa ili kukua. Kitu ambacho sio cha kawaida (Magic) kinakuja wakati mbegu hii inayopandwa inaweza kukua.
Ikiwa watu wote wangeweza kugundua Upendo ndani yao, wangeweza kusaidia kujenga daraja pale ambapo kuna ugomvi na kufuta hisia za chuki zilizopo katika Dunia.
Kutahajudi kwenye Mwanga na Sauti kuna uwezo wa kuonyesha Upendo wa Mwisho unaojumuisha kila kitu na kila mmoja kwa umoja mkamilifu.
26 Januari 2019
Huu ni ujumbe kutoka kwa Mabwana wa Mwanga
Uzuri katika dunia upo kwa wote kuona, iwe kuwa ni kutoka kwa viumbe wadogo sana mpaka kwa utukufu wa mlima. Hazina duniani zinaweza kuonekana na kukubaliwa na kila mtu. Hata hivyo, kulingana na maoni yetu, watu wanaonekana kuwa na nia kwa hazina nyenzo zaidi.
Sisi tunafahamu sana kwamba ni rahisi kuweza kufungwa na tamaa ya kile ambacho pesa inaweza kununua. Lakini hizi sio hazina za kudumu na zitatupiliwa mbali wakati jambo lingine linapokuja.
Wakati ni wa thamani sana, hasa kwa teknolojia ya kisasa mtu anaweza kwa urahisi kupata wasiwasi na mitandao ya kijamii na mambo mengine mengi ambayo yanapatikana kwenye kompyuta.
Watu wanasahau dunia ya nje, wanasahau kuzoea uzuri wa Asili (Nature), na kuwa na ufahamu wa furaha ya kuwa mashambani. Kuwa nje husaidia kupunguza kasi ya watu kutoka kwenye kukimbia na hekaheka ya dunia ya leo. Inakuruhusu wewe “Kuwa” tu na, sio “Kutenda” – mapumziko kutoka kwenye dunia yenye hatari ambayo muda uko kama hakuna “masaa ya kutosha katika siku”.
Kwa hiyo ni muhimu kubadilisha tabia na myenendo yenu, ikiwa ni muhimu, ili kutenga wakati kwa ajili ya kuwasiliana na Asili. Maisha yenu yatatajirishwa, sio kwa faida nyenzo lakini kwa kitu cha thamani zaidi – kwa kulisha Kuwa kwako kwa Ndani – na kukufanya kuwa na Heri zaidi, Furaha na Kutosheka.
14 Januari 2019
Huu ni ujumbe kwenu wote kutoka kwa Mabwana wa Mwanga.
Tumekuwa tunasubiri wakati huu. Sasa ni wakati wa kupata watu wengi kutahajudi iwezekanavyo kila siku. Hii Tahajudi ya Pamoja itakuwa na athari kubwa sana katika Dunia. Tafadhali wasilianeni na watu wengi kama mnnavyoweza ili kuwajumuisha.
Kutoka kwenye mtazamo Wetu, wakati watu wakifanya hivyo kwa wakati mmoja, Tunaweza kuona mwanga unavyoongezeka na kuenea Dunia yote.
Wakitahajudi watu zaidi, Nguvu zaidi na Kiwango huongezeka.
3 Januari 2019
Kifo ni swala la udadisi na utata ambalo hakuna mtu anayeelewa kweli, ni kama kuzaliwa vilevile – “Tunatoka wapi na tunaenda wapi”.
Watu wana wasiwasi na hawavielewi kiasi kwamba hawataki kuzungumzia kuhusu kifo au kuzaliwa kwa kina. Hata hivyo ni jambo moja ambalo litatokea kwa kila mtu.
HAKUNA KITU HALISI NA HAKUNA KITU KILICHO KAMA KINAVYOONEKANA!
Sisi “tunatabasamu” mara nyingi wakati watu wanashikilia mali zao, kwani kweli hakuna kitu cha mtu yeyote. Mali za kidunia zinapaswa kuachwa nyuma. Wanapaswa kutafuta mambo dhahania ambayo ni ya kudumu: Upendo, Faraja, Amani, Utulivu, Furaha, Kutoa, Ajabu, Uzuri.
Hizi ni sifa za Milele na kamwe hazitapotea.
1 Januari 2019
Hapa ni Mabwana ya Mwanga tunawaletea Ujumbe Wa Mwaka Mpya.
Tunafuraha sana kusema kwamba ingawaje watu wengi katika dunia bado wanaishi maisha yao bila kujua madhumuni yake, kuna idadi kubwa ya watu ambao hatimaye wamepata sababu ya kweli ya maisha yao.
Kutahajudi kwenye Mwanga na Sauti ya ndani huongeza mara moja Ufahamu wako, na kutokea hapo inawezekana kuishi maisha yako kwa mtazamo tofauti kabisa.
Kuna idadi kubwa ya vitabu huandikwa, na semina zinazotolewa ambazo zinaonyesha njia zenye msukumo sana wa kuweza kukabiliana na changamoto za maisha – jinsi ambavyo inawezekana, kwa kubadilisha mawazo yako tu na mwelekeo wa tabia, kuendeleza njia mpya ya kuwa kwako ambayo inatosheleza.
Lakini, nini kinatokea wakati kitabu kimeshasomwa na semina kusikilizwa na kueleweka? Kwa kawaida watu hurudi nyuma na kuendelea na njia za zamani za kukabiliana na hali na mihangaiko ya maisha inawachukua tena.
Kinachohitajika kwa wale wote ambao wanatafuta “majibu” ni kitu kudumu zaidi.
Kuanzishwa au kupata “Initiation” kunamrumhusu Mtahajudi kupata majibu mwenyewe. Kila wakati wanapo Tahajudi Nguvu ya Mwanga na Sauti itaenea na kuwa kwenye kiini cha msingi wao, na kuruhusu kina cha Maarifa ambacho bado hakijatumika. Uhuru mpya sasa umepatikana, Mtahajudi hajafungwa tena ndani ya mipaka ya mwili “physical body”.
Kama umekuwa na bahati ya kupokea huu “Muujiza” basi usiwe nao mwenyewe – waambie wengine, ili Muujiza huu uweze kutimiza maisha yao pia.
19 Desemba 2018
Huu ni ujumbe kutoka kwa Mabwana wa Mwanga.
Wakati tunafikia mwisho wa mwaka na kuanza mwaka mpya daima ni vizuri kutafakari juu ya matukio yaliyopita na jinsi ambavyo mwaka mpya utavyokuwa.
Kama ilivyotabirika, mwaka huu Lightwave Mpya imevutia maelfu ya watu ambao wameanzishwa (Initiated) na wengi kupata Ukombozi wa Ufahamu (Enlightenment).
Baadhi ya watu hawa wana uhusiano na mawasiliano moja kwa moja na sisi na wamepokea ujumbe. Mara nyingi ujumbe umekuwa zaidi wa kibinafsi.
Hata hivyo, sasa kutakuwa na watu ambao watakuwa na habari muhimu kuhusu Ascension. Habari hizi inabidi kusambazwa kati yenu ili kila mtu ajue kinachoendelea.
10 Desemba 2018
Hii kutoka kwa Mabwana wa Mwanga.
Wewe unatuomba Sisi kueleza kuwa Uongozi wa Kiroho ni nani, ili watu waweze kuelewa zaidi kuhusu chanzo cha Nishati na nguvu inayoendesha Njia ya Mwanga na Sauti.
Sisi ni Masters tuliopaa “Mbinguni” ambao hukusanyika katika Ngazi za Juu za ulimwengu wa Kiroho kwa madhumuni ya kusaidia binadamu tu. Bila shaka, kuna haja ya kuwa na uhusiano na mawasiliano duniani ili ujumbe uweze kufika. Ngazi za Juu za ulimwengu wa Kiroho ni makazi ya Viumbe wengi, wengi ambao hawajawahi kuchukua miili ya kibinadam.
Ni vigumu kwa watu, kwa kweli kuelewa nini Tunafanya. Jambo bora ni kutuona sisi kama Viumbe Wema ambao wanaweza kupatikana na kuwasiliana na kuongoza watu katika njia ya Ukweli na Wema. Mabwana ya Mwanga na Masters waliopaa ni sawa.
Jinsi ambavyo watu zaidi na zaidi wanasikia Sauti na kuona Mwanga bila kutegemea, kuna wale ambao wanaweza kusaidia kuelewa hili. Dunia inabadilika, ingawa kuna uchoyo sana, watu wanatambua kuwa mambo ya udongo (material) waliyoyatafuta hayana maana katika kueneza Ukweli kupitia Kutahajudi.
3 Desemba 2018
Hii ni kutoka kwa Mabwana ya Mwanga.
Unyenyekevu. Hii pengine ni suala muhimu zaidi la kuendeleza katika maisha ya watu. Zamani hili lisingekuwa tatizo, kwani hapo zamani za kale watu kwa ujumla walikuwa na maisha ya msingi na rahisi sana.
Lakini sasa, mambo yamebadilika kwa kiwango kikubwa. Ni vigumu sana kutokuwa na mvutano na shikinizo kila siku, kuhusu kufanya maamuzi na matatizo yanayowakabili watu Duniani.
Lakini kuna ufumbuzi wa tatizo hili. Tabia na mazoezi ya kutahajudi yataleta, baada ya muda, yatahamasisha maisha rahisi na yenye maana zaidi. Haitatokea kwa siku moja, lakini utaratibu wa kuweka muda wa kukaa tu kwa raha na kutahajudi, utasaidia kufanya mabadiliko haya.
Hatimaye wakati utakapofikia madhumuni yako ya kweli, mambo ambayo yalionekana kuwa muhimu yataangukia mbali, na kuacha hali ya amani na utulivu.
18 Novemba 2018
Sisi ni Mabwana wa Mwanga. Tuko hapa kuzungumza na nyie kuhusu mamia ya watu ambao sasa wanaona Mwanga wa Kiroho bila kutarajia wakati wanatahajudi.
Si lazima kuwa wazoefu wa kutahajudi kwa hili kutokea. Mwanga inaonekana tu. Kwa sababu ya Mwanga mwingi wa Kiroho kwenye Sayari hivi sasa, watu wanakuwa na uzoefu wa kuona Mwanga kabla ya kupata Initiation.
Kama hii inatokea, watahajudi lazima kuangalia tu na kuacha kila kitu “kuwa” bila uchambuzi. Ni muhimu kuwa na mazoezi ya kufanya hivyo katika maandalizi kwa ajili ya tahajudi za juu zaidi baadaye.
7 Novemba 2018
Hii ni kutoka kwa Mabwana wa Mwanga.
Tafadhali kumbukeni kuwa sisi tuko hapa kuwatumikia binadamu kwa njia yoyote ile Tunayoweza. Kwa sababu mbalimbali watu wengi wanakuwa na maisha magumu sana na/au kuhisi huzuni na upweke.
Wakati Ascension inakaribia sana ni muhimu kuwa na uhusiano mzuri na Sisi ili Tuweze kuwasaidia watu kwa majeraha au matatizo yoyote – au hata kutoa ushauri kwa jumla.
Watu wengi wanafikiri kwamba inabidi kuwa “peke yao” maishani bila msaada wowote lakini hiyo si kweli kabisa. Siku zote kuna msaada na kinachohitajika tu ni kuuliza na kuomba msaada.
Fikiria binadamu wenzio – kuwa na ufahamu kuhusu matatizo yoyote wanayoyakabili. Zungumza na watu wenye upweke, kuwa na huruma na toa msamaha wa wema na upendo.
Ni kwa kufanya mambo haya rahisi, kama ambavyo watu wamefundishwa kwa miaka mingi, ambapo binadamu watafikia kilele cha asili ya huruma na kuishi kweli maisha yao wakiwa na Upendo mioyoni mwao.
17 Oktoba 2018
Hii ni kutoka kwa Mabwana wa Initiation.
Initiation tunayoongelea kwenye kurasa hizi haiwezi kueleweka kikamilifu mpaka watahajudi watakapokuwa na ufahamu wa ndani wa Mwanga na Sauti kwa miezi kadhaa.
Ni kana kwamba mlango wa Kiroho umefunguliwa, lakini Watahajudi bado “kuingia na kupita” kwenda kwenye ulimwengu wa Kiroho ambao hapo awali hawakuwa wanaufahamu. Ni siri kamili kwao!
Kabla ya Initiation mtahajudi inamlazimu awe na tabia njema kuhusu kutahajudi. Sio kazi rahisi, lakini kama mazoezi yanafanyika, basi watakuwa na uwezo wa kuwa na ukawaida, hata wakati mambo yanapokuwa magumu, ama kwa mabadiliko ya maisha au kama wanahisi tahajudi zao haziendi vizuri.
Kama ilivyosemekana mara nyingi kabla, faida ni nyingi na mbalimbali. Kufuata Njia ya Kutahajudi kwenye Mwanga na Sauti, ni Safari itakayoishia na kusababisha furaha kamili na amani yote.
Ni watu wangapi hutafuta hili katika Dunia ya kisasa?
14 Oktoba 2018
Ni Sisi, Mabwana wa Mwanga.
Tunapoongea kuhusu Upendo katika mfumo wa juu, Tuna maana kile ambacho hupatikana kwenye Enlightenment. Watu hutumia hili neno kwa uhuru sana sasa, wao wana upendo wa hiki au upendo wa kile.
Lakini, kama ukipata Initiation na Kutahajudi kwenye Mwanga na Sauti, basi maana inakuwa na kina zaidi. Initiate huenda katika Safari ya kushangaza na ajabu inayowaongoza wao kwenye Chanzo cha Uumbaji. Upendo unaopatikana, kama watu Wakitahajudi zaidi na zaidi, unapita zaidi sana upendo wowote wanaojisikia kwenye Ulimwengu wa Kimwili.
Upendo wanaohisi kwa familia zao kwa mfano unapitwa kabisa na Upendo wanaohisi ndani wakati wao wanaTahajudi. Jambo la kufurahisha ni kwamba wana uwezo wa kuleta Upendo huu katika maisha yao ya kila siku, ambayo vilevile yanakuwa tajiri na ya maana zaidi.
10 Oktoba 2018
Sisi ni Mabwana wa Mwanga.
Kama mnavyoweza kufikiria, Sisi tunaona mambo mengi kuhusu
binadamu. Ni muhimu kukumbuka kwamba hamhukumiwi – ila kuangaliwa tu.Lakini Sisi huguswa wakati Tunaona mambo ambayo mnaweza kufanya ili maisha yenu / Tahajudi zenu kuwa rahisi na za kutosheleza zaidi.
Ni vigumu kufikiria jinsi gani ilivyo kuishi katika umaskini uliokithiri, wakati hujui hasa hata chakula utapata kutoka wapi. Lakini kuna mamilioni ya watu wanaoishi namna hii, wanaishi maisha duni ya kila siku bila mapunziko.
Kwa wale walio na hali bora ya maisha ni tofauti sana. Mahitaji ya msingi yameshakamilika, sio kama walio na maisha duni ambao wanapambana kuishi.
Moja ya vikwazo vikubwa ambavyo watu inabidi kukabiliana navyo ni ukosefu wa shukrani. Hii inapaswa kuendelezwa kuanzia umri mdogo hivi kwamba wakati wa kufikia utu mzima shukurani imekaa akilini kabisa.
Kila siku, shukuru kwamba mahitaji yako ya msingi yamekamilika!
Kila siku, kushukuru kwamba wewe ni hai na kuwa na chakula cha kutosha!
Kila siku, kushukuru kwamba una nyumba na mahali pa kuishi!
Mambo haya ya muhimu ndiyo jiwe la msingi ambalo kila binadamu anapaswa kuwa nalo kama msingi wa kuwepo kwake. Cha kusikitisha, hivi sivyo ilivyo. Kwa hiyo, wakati unatoa shukrani, tuma Upendo kwa wote walio katika mateso na maumivu. Kwa kufanya hivi inasaidia kukufanya wewe kutambua kuwa ingawa inawezekana kuwa huna vyote unavyotaka – kweli unavyo vyote unavyohitaji. Hii itakufanya wewe kuwa mtu bora zaidi.
5 Oktoba 2018
Sisi ni Mabwana wa Mwanga tunazungumza na nyie wote.
Mengi yanaweza kupatikana wakati mnajitahidi “kukaa kwenye mto” (kutahajudi) kwa muda mrefu zaidi. Jaribu kutumia wakati huu kwa busara na kujaribu kabisa kujisalimisha kwenye Mwanga na Sauti.
Huu ni muda wako wa kuwa mbali na shughuli zako za kila siku. Sisi daima tuko hapa kuwasaidia na kuwaongoza, hivyo tafadhali ombeni. Inaweza kuwa kwa msaada wa Tahajudi zenu, au baadhi ya masuala ya kidunia ambayo yanawatatiza.
Sisi kweli tunataka sasa watu watengeneze uhusiano na sisi. Hii inaweza kufanyika kwa kuchukua muda wa dakika chache za muda wako wa Kutahajudi kila siku, na kuzingatia kwenye jina letu: Mabwana wa Mwanga.
2 Oktoba 2018
Hii ni kutoka kwa Mabwana wa Mwanga. Sisi tunatuma ujumbe huu wa kuwapa Tumaini na msukumo kwa wote ambao wangependa “kesho” kuwa bora – wale ambao wangependa kuona Binadamu wanaelewana kwa ajili ya manufaa ya wote.
Tahajudi ya Lightwave ambayo inafundisha Upendo, amani, unyenyekevu na huduma, msingi wake ni Njia ya Tahajudi ya Mwanga na Sauti. Hii imekuwa ikifundishwa kwa karne nyingi kama njia ya kujiunga pamoja kama “kitu” kimoja. Kila mtu ana fursa ya kupata Mwanga na Sauti ya ndani ambayo ni Chanzo cha Kiroho.
Pamoja na watu kujifunza kuhusu jukumu lao katika mchezo huu mkubwa wa maisha, wakati watu zaidi na zaidi wanapata Nguvu hizi, itakuwa na “athari nzuri” kubwa juu ya Dunia kwa jumla – itabadilisha jinsi watu wanavyofikiri, wanavyohisi na tabia zao.
15 Septemba 2018
Sisi, Mabwana wa Mwanga, tunapenda kutoa ujumbe ufuatao kwa Watahajudi wote.
Tunayo furaha kubwa kuwasalimu, kama wanachama wapya wa Lightwave Mpya. Sisi tunanyenekea kwa kuona kiasi cha kazi ambacho ninyi manafanya, kuhakikisha kwamba kundi hili, ambalo Hutahajudi kwenye Mwanga na Sauti, linakua na kufikia watu wengi sana Duniani kote.
Hatuwezi kusisitiza ya kutosha umuhimu wa kuwaongoza watu kwenye Njia ya Kutahajudi. Kadri wanachama watakavyoongezeka mtagundua mabadiliko makubwa kuhusu jinsi watu wanavyofikiri, wanavyohisi na tabia zao. Upendo Utaenea na kuwa na uwezo wa kuathiri idadi kubwa ya watu.
Kama tulivyosema hapo awali, Lightwave Mpya siyo Njia pekee ya Kutahajudi, lakini ndio yenye Nguvu Nyingi zaidi na uwezo wa kubadilisha Hali za Ufahamu wa watu, kwa njia ambayo haijawahi kuonekana tena.
Kwa hivyo kuweni macho na waambieni marafiki na familia zenu. Fikiria ni jinsi gani utaleta furaha kwa watu hawa. Kisha nao wana nafasi ya kugundua kile ulicho nacho, kuna uwezekano gani tena wa zawadi kubwa zaidi inaweza kuwa?
January 3, 2018
Upendo ni Kila Kitu
Upendo ni mwanzo, kati na mwisho.
Hakuna mahali ambapo Upendo haupo.
Upendo, kwa maana ya juu, ndio sababu ya kila Kitu kuwa.Sisi Mabwana wa Mwanga tuko hapa kwa majadiliano juu ya jinsi ya kuunganisha Upendo katika maisha yenu ya kila siku.
Sisi hatuzungumzii juu ya upendo wenu kwa familia zenu na marafiki, au upendo wa maeneo mnayopenda kutembelea, filamu mnazopenda kuangalia, kwa maneno mengine upendo unaotimiza mahitaji yenu ya kihisia ya kila siku.
Kwa kuwa sasa mmekuwa Initiated katika Nuru na Sauti “Dunia” nzima mpya imefunguliwa kwenu. Wakati unapotahajudi kwenye Nishati hii unaleta Upendo kutoka Chanzo cha Juu kuja ndani yako mwenyewe hasa. Hii ndio sababu Tunawaomba kupitasha Upendo huu wa Juu kwa kila kitu sasa kwenye Ulimwengu.
Upendo wa duniani una mipaka yake; ni vigumu kumpenda mtu au kitu ambacho hatujakiidhinisha.
Upendo ambao tunaoongelea ni wa Milele, hauna Mipaka, hauna Kikwazo. Wakati kweli ukielewa hili, ni rahisi kuondoa mipaka iwazungukayo ambayo mnajiwekea karibu yenu. Mnao uwezo wa kuwa na Upendo kwa ombaomba wa mitaani au watu usiowaheshimu, kwa kweli unaweza kuwa na Upendo wa vitu vyote, watu na mahali.
Hebu fikiria itakupa uhuru kiasi gani. Fikiria Nguvu unazotumia katika kutopenda hiki au kile. Ni kama gamba limefunuliwa na hatimaye unaweza kukubali kila kitu kwa Upendo na msamaha.Upendo mnaotuma kila siku kwa Sayari ni kuwasaidia watu kupata Upendo ambao wamepoteza. Lakini pia ni kufanya mazoezi ya Upendo wa Kila kitu bila kuhukumu.
Huko ni Kupenda Kweli.
Desemba 23, 2017
Sisi ni Mabwana wa Mwanga tunawapa ujumbe wa Krismasi. Wakati Krismasi inakaribia tunakumbushwa hadidhi ya eneo la hori ambayo inazungumzia juu ya kuja kwa Mwalimu mkubwa.
Ingawa hadithi sio sahihi kabisa, ujumbe ni …… Upendo, Amani na Wema kwa watu wote. Mwalimu huyu mkubwa aliweza, kwa wakati wa muda wake mfupi duniani, kukusanya timu ya wafanyakazi na hatimaye kueneza mafundisho yake duniani kote.
Ni wakati mwingine tena wa kufanya jambo kama hilo. Sisi, kwenye Uongozi wa kiroho, tunafahamu sana kwamba hii si kazi rahisi. Kwenye Dunia iliyojaa uchoyo, mashaka na giza mnahitaji kubadili na kurejesha kukubalika, Upendo na Mwanga.
Kwa kufanya bidii na kazi ngumu na uamuzi kamili wa watu wengi ambao wanataka kusaidia kueneza Lightwave mpya, mipaka inavunjwa. Sisi tunafuraha katika kile kinachoendelea na maendeleo ambayo yanafanyaka.
Hakuna kitendo cha wema, hata kikiwa kidogo namna gani, huenda bila kuonekana na ninyi ni Nyota ambazo huleta Mwanga kwa Duniani tena.
Oktoba 15, 2017
Sisi, Mabwana wa Mwanga tutakuwa tunatoa baadhi ya maneno ya msukumo juu ya Initiation – ni lazima ionekana kama siri, vinginevyo Initiate wataona kama zoezi la akili na watashindwa “kujiachia” na kuwa katika Utukufu na Uzuri wa yale yanayoweza kuonekana.
Ni lazima pia isemekane kuwa kile kinachoonekana kinamuonyesha “Initiate” mambo anayohitaji kujifunza ili kukua na kuendelea mbele. Nguvu ya Mwanga na Sauti ni Mwalimu kamili, Anajua nini hasa mwanafunzi anahitaji na huendelea kumuonyesha mpaka mwanafunzi anaelewa.
Kupata Initiation kwenye Njia ya Kiroho kwa njia ya Mwanga na Sauti inahusu kujifunza na kukua. Ndiyo, unaweza kuona matukio ya ajabu njiani – lakini jifunze kuona na na kuachia, badala ya kuwa umefungwa na kuchukuliwa na vielelezo.
Kama kwenye maisha, kama unashiriki sana katika jambo lolote lile wakati mwingine unaacha kuendelea. Kwa mfano, unaweza kuwa unafanya kazi usiyoipenda na una haja ya kubadilisha. Mwanga na Sauti utakuonyesha njia kama ukiuuliza. Daima uuliza!
Oktoba 1, 2017
Ni lazima ieleweke kwamba Kila kitu ni Kimoja – Hii ni Kanuni ya msingi. Kila chembe ambayo inafanya Ulimwengu kwa ujumla huja kutoka Chanzo hicho ambacho kinaweza kujulikana kama Mungu.
Ukifuatia Kanuni ile ya msingi inamaanisha kuwa Kila kitu katika Ulimwengu ni Kimoja – ambacho ni Mungu. Kwa kuwaunganisha watu na Mwanga na Sauti inamaanisha kuwa wao Wanatahajudi kwenye Kielelezo na Ufunuo wa kile Chanzo. Na inaweza kusemekana kwamba watu kweli Wanatahajudi kwao Wenyewe, kwa maana ya sehemu ya Juu ambayo ni Wao Wenyewe.
Hii ni safari ambayo huchukuliwa na mtu binafsi kutafuta Hali Asili (Nature) yake ya kweli – ambayo ni ya Mungu.Mtahajudi ana uchaguzi wa “kuachia” kila kitu kinachompa wasiwasi duniani. Kama wakifanya hivyo basi Safari yao itakuwa rahisi na watafikia Chanzo (Enlightenment) kwa haraka na kwa urahisi. Mtu anayechukua hofu na wasiwasi tu kwenye Tahajudi yake hatakuwa na wakati rahisi. Wanaweza kuwa na tatizo katika kuwasiliana na Nguvu (Mwanga na Sauti) na kuhitaji msaada kutoka kwa Watahajudi wenye uzoefu zaidi.
Kwa vyovyote vile Lengo linaweza kufikiwa. Ufanamu kamili na uhusiano na Chanzo ni zaidi ya kitu chochote ambacho wamewahi kuwa na uzoefu nacho kabla. Furaha, Amani na Upendo ambavyo Havipimiki na Haviwezi kuelezeka au kueleweka.
Kuna sababu nzuri kuwa, na ndiyo maana imeitwa “Amani inayopita ufahamu wote”.
Agosti 23, 2017
Hapa ni tofauti – hamuwezi kufikiria – ninaona kwa jicho linaloona kila kitu na ninaweza kuona kila kitu kwa wakati mmoja – na kuelewa yote. Kila mtu inaendeshwa na ajenda zake mwenyewe ambazo walitengeneza tangu kuzaliwa kwao – wakati mwingine / mara nyingi zikigongana na ajenda za watu wengine. Mara nyingi tanabasamu kwani migongano hii mara nying haina sababu kwani inaletwa kwa ajili ya kutoaminiana bila sababu au kutokuelewana.
Hivyo kwa namna hii pia Ascension mara nyingi inasemekana kutengenezwa na watu ambao wanadhani wanajua hili na lile. Ascension Inatokea hivi sasa wakati watu wanakuwa na ufahamu wa matukio yalilyokuwa siri awali.
Taratibu wonyesheni na kuwaongoza watu kwenye Njia ya Kujua.
Agosti 21, 2017
Tunahitaji kuangalia zaidi sasa kuwahamasisha Initiates kuwa na moyo, sio wa kutuma tu Upendo kila siku kwa Sayari na wakazi wake, lakini pia kwa wao wenyewe na kila mmoja wao.
Toa msamaha wakati mtu anakukosea na jaribu kuwa na huruma kwao. Na sio rahisi na hupaswi kuwa kama janvi, lakini wakati mwingine ni bora tu kuacha mambo yalivyo na kumkubali mtu mwingine kama alivyo badala ya kupambana naye.
Jaribuni kufanya maisha yenu ya Duniani kuwa rahisi kwa kuondoa chuki na hasira kwenye miyoyo yenu. Kila mtu ana Karma yake mwenyewe ya kukabiliana nayo na wakati mwingine hawawezi kujizuia kuwa na tabia kama walizonazo.
Daima chagua Amani, sio vita.
7th February 2017
Tungependa kuwapongeza watu wote, haswa wale wa Amerika ya Kusini na Afrika, ambao ndiyo kwanza wameanzishwa kwenye Lightwave. Wengi wenu wamekuwa Second Initiates na Adepts.
Kwa kuwa mmeendelea haraka kwenye Njia ya Kutahajudi, inamaanisha kuwa watu wengi zaidi wana uwezo wa kuleta chini Nguvu za Kiroho zinazohitajika ili kusaidia katika kuongeza Ufahamu wa Sayari na kutoa “negativity”.
Kila wakati ukikaa chini na Kutahajudi, kumbuka kuwa sio kwamba unasaidia kuleta chini Busara na Maarifa kwako mwenyewe tu, lakini unaleta chini Mwanga mkubwa wa kuondoa giza la Dunia.
Kama wewe ni Initiate wa Kwanza au umeendelea zaidi, jaribu kujitahidi kadri kwa uwezo wako kuwa katika wakati kikamilifu kwenye Tahajudi yako kila siku na kutuma Upendo na Mwanga Duniani kote.
.
1st January 2017
Tunapenda kutuma ujumbe ufuatao wakati Mwaka Mpya unaanza kwenu.
Ni kwa furaha kubwa kwamba sisi tunaona Dunia inakuwa na Mwanga, wakati wengi wenu mnatahajudi, wakati wa kipindi hiki cha Neema.
Adepts wapya, First Initiate na Second Initiate kati yenu inabidi kuimarisha Utambuzi wa Hali zenu. Na kama inawezekana kutumia muda kutafakari juu ya Hali zao mpya za Kuwa na kweli nini maana yake. Usiwe na haraka ya kujihusisha na masuala ya kidunia, kuwa katika mapumziko na Utulivu tu kwa muda mrefu kama kadri ya uwezo wako.
Kwa ninyi wenyewe kuwa imara mtaweza kuwa kioleza cha Mwanga na mfano kwa wengine. Onyesha wema kwa kila mtu. Jaribu kuhukumu lakini kutuma Upendo na kupata Beauty na mapumziko na utulivu kwamba anaishi katika nyote. Kuwa Shupavu kwa watu wengine inapokuja suala la kuzungumza juu ya uzoefu wako kwenye Njia ya Kutahajudi.
Onyesha Hekima.
Sema Ukweli wako
Onyesha Upendo na Huruma kwenu wenyewe na wengine.
5th December 2016
“Ni kana kwamba Mwanadamu kwa namna fulani ameinuliwa, kuwa na uwezo wa uwezo kuendelea na maisha yao wakiwa na Nguvu zilizoongezeka zaidi. Ina maana kwamba watu kweli watakua na Kupanda tu kama wako tayari na itakuwa uteuzi binafsi.”
25th November 2016
“Sasa ni wakati wa utekelezaji. Zaidi na zaidi watu wanakubaliana na wazo kwamba kuna mabadiliko yanaendelea, lakini hawana uhakika kwa namna gani au wapi itatokea. Tunahitaji kukuambia kuwa kuna watu duniani kote ambao ni hisi kwamba wanahitaji Uongozi wa Kiroho na wangependa kusikia kuhusu Tahajudi ya Mwanga na Sauti.
Dunia iko tayari kwa hili SASA HIVI.”
24th November 2016
“Sasa Tunahitaji kushughulikia wazo kwamba watu wataachwa nyuma wakati mabadiliko ya kasi ya mtikisiko (vibrational frequency) yatakapotokea, mabadiliko makubwa ambayo yanahitaji watu kuwa wazi sana kwa njia tofauti ya maisha na kuishi.
Kama watu ni wajeuri na wana wazimu wa madaraka basi wataona mabadiliko kuwa magumu mpaka watakapofuta hisia hizo. Vile vile kwa watu wabinafsi, na wale walio na aina ya mielekeo hiyo na mingine basi itakuwa vigumu kuzitokomeza.
Watu hawa hawatafaa katika Dunia hii mpya iliyojaa Upendo na Amani. Kuna muda bado kwa watu hawa kubadilika na kuona makosa ya mienendo yao, kwa hivyo wana haja ya kuchukua nafasi hii sasa!
Ndiyo maana ni muhimu sana kuzungumza na wengine kuhusu mazoezi ya kila siku ya Kutahajudi.”
24th November 2016
“Kama ilivyoelezwa – kuongeza Ufahamu wa watu ni muhimu. Kidogo kidogo utaona mabadiliko jinsi ambavyo watu wanavutwa kuelekea kusaidiana na kuvutiwa zaidi na mambo ya Kiroho. Inaweza kuonekana kama mapambano zaidi hapo mwanzoni, lakini wakati idadi fulani ya watu wameunganishwa na Mwanga na Sauti kutakuwa na mawimbi ya furaha na mshangao kwa jinsi ambavyo kuna Upendo na Amani zaidi Duniani.
Tunahitaji Mataifa yote ya kushiriki, baadhi yao kwa kiasi kikubwa au kidogo. Watu wote ambao wameunganishwa sasa wanahitaji kuzungumza na wengine, na hivyo kufanya watu kutambua kinachoendelea. Ni muhimu kwamba hii itokee, na sio sana kuhusu Hali ya Kiroho ya mtu binafsi lakini Nguvu ya watu wengi waliokuwa Enlignhtened ambao wataleta mabadiliko ya kweli. Kwa sababu wao Wanatahajudi na kuleta chini Nguvu za Kiroho zitawatia moyo wengine kufanya hivyo.
Wakati idadi ya watu wa kutosha ikifikiwa itakuwa ni wakati wa kuongeza kasi ya mtikisiko (vibrational frequency), hata hivyo, ina maana kwamba watu wengi wataachwa nyuma -. hawataweza kuwa sehemu ya mabadiliko haya mkubwa yatakayofanyika”
22nd November 2016
“Tunahitaji sasa kuzungumza juu ya kuongeza ufahamu. Inamaanisha nini? Naam, mtu wa kawaida anayeishi katika Dunia ya leo anapata vichochezi mbalimbali. Yeye anaweza kuona karibu yake maajabu ya Dunia na kusikia sauti nyingi.
Lakini nini kitatokea kama ghafla atakuwa na jozi zaidi ya macho na ya masikio – au kuchochewa hivi kwamba angeweza kuona na kusikia mambo ambayo hat sasa bado hayajatambuliwa, ni jinsi gani ingekuwa ajabu? Ni wazi kuna njia bandia za kufanya hivyo, kwa madawa n.k..
Tahajudi ya Mwanga na Sauti haifanyiki kwa madawa ya kulevya, lakini ni Ufunuo ili kumpa mtu upatikanaji wa Maarifa ya ulimwengu wa Kiroho – ambayo pia itaongeza Uelewa wa Ufahamu wake wa kuelewa zaidi mahali pake na kuhusu utendaji wa ndani wa Ulimwengu.”
22nd November 2016
“Kila kitu kina mawimbi na mtikisiko (frequency) – hata Dunia yenyewe. Ni kama mwongozo wake au sahihi. Kila mtu, mnyama, hai au asiye hai, kila kitu kinatikisika katika mzunguko na mawimbi yake ya kipekee. Hakuna kinachotikisika kwenye mtikisiko (frequency) moja. Kidogo ni kama chembechembe ya theluji, kila mmoja ni ya aina yake yenyewe, hakuna chembechembe mbili ambazo ni sawa.
Kama tukimchukua Binadamu na kuongeza Ufahamu wao kwa Kutahajudi kwenye Mwanga na Sauti, ili kwamba awe Enlightened haitabadilisha mawimbi na mtikisiko (frequency) au mwongozo wake wa awali.
Kama hata hivyo, mawimbi na mtikisiko (frequency) wa dunia na wakazi wake inaongezwa, Binadamu watakuwa watajiendesha katika ngazi ya tofauti kabisa – ambayo ina maana njia nzima mpya ya maisha. Itakuwa vigumu kufikiria jinsi ambayo itakuwa. Kuna mengi zaidi yanakuja juu ya mada hiyo, lakini kwanza ni lazima kuangalia mambo yalivyo kwa sasa.
Tunahitaji kuongeza Ufahamu wa pamoja ya Sayari ili watu wawe tayari kwa ajili ya mabadiliko hayo makubwa. Inaonekana na kusikika kama ndoto lakini kile tunachozungumzia ni umoja wa Dunia ambapo Upendo utashinda.”
Novemba 21, 2016
“Watu wengi kwenye maisha hawana muda kabisa – wanahitaji kujisikia kana kwamba kuwepo kwao kuna maana kwa kujaza kila dakika ya wakati unaopatikana. Hata husema kwamba hakuna masaa ya kutosha katika siku moja kumalizika kila wanachohisi wanahitaji kufanya.
Wakati kazi zao zimefanyika wao hawawezi kupumzika kwa sababu kiasi kikubwa kingine cha kuchochea hisia. Kama mtu hawezi kupata muda kila siku wa Kuwa tu, kupumzika na Kutafakari basi maisha yao yatakuwa muda mmoja mrefu wa mapambano. Kwenda kutoka shughuli moja hadi nyingine bila mapumziko katikati haiwasaidii aidha wenyewe au familia zao.
Mtu anahitaji ule wakati maalum wa kutulivu akili zao na kuwa huru bila wasiwasi. Mazoezi ya Kutahajudi kila siku ni mazuri na kamili kwa sababu watu wanaweza kujengea na kujiongezea muda hatua kwa hatua. Kila wanavyofanya zaindi ndivyo wanavyopata faida zaidi; ni formula ya ajabu.
Hii ni ugonjwa mkubwa katika dunia leo – usimamizi wa muda. Watu hawajajiachia muda wa kutosha kuandaa muda wao bora! Kwa hiyo wanachukua muda wa usiku kufanya mambo ambayo hawajafanya wakati wanapaswa kulala.
Ujumbe ni wazi – Kutahajudi ni jibu la matatizo mengi duniani. Kama kila mtu akifanya aina fulani ya Kutahajudi/Kutafakari basi sisi tungekuwa na msingi wa maisha ya furaha, zaidi na ya kutosheleza kwa watu wote. ”
Novemba 21, 2016
“Dunia ni mahali pa giza sana kwa watu wengi na kunahitajika mabadiliko makubwa. Maandiko mengi ya zamani ya dini ya zamani na mafundisho huzungumzia hili na kutaja kuwa kutakuwa na Nguvu kutoka Juu kuathiri mabadiliko muhimu sana yanayohitajika.
Kuleta Upendo kwanye Sayari ndio njia pekee ya kufanya hivyo – upendo duniani kwa sasa hauna nguvu ya kutosha ya kuondolea mbali uyakinifu, nguvu na kupenda madaraka na ugonjwa unaoshinda.
Kinachotakiwa ni Upendo Usio na kikwazo, Upendo wa aina ya nguvu zaidi ambao unaweza kukata na kupunguza ugomvi wowote ule na kuleta amani ambayo itainyanyua Dunia kwenye Ngazi nyingine.
Upendo Usio na kikwazo ambao mimi nauongelea unaletwa chini kutoka ulimwengu wa Kiroho na watu wengi wanakuwa na uzoefu wa Nguvu hii kubwa na kushuhudia wenyewe athari yake, kwa njia ya Enlightenment.
Kutakuwa na ongezeko kubwa la idadi ya watu watakaopata Enlightenment kila mahali Duniani na kwa hiyo watakuwa na uwezo wa kugawa Upendo huu ambao ni wa Kujumuisha kila kitu na Vitu Vyote. ”
Novemba 20, 2016
“Je, umeshawahi KWELI kujiuliza ni jinsi gani mwili unaweza kweli kusogea; mnyama mwenye uzito wa tani, jinsi gani uzito huo mkubwa unajichukua na kusogea wenyewe? Maajabu ya Dunia ni makubwa sana Kuyatafakari lakini ningependa ujaribu – kutambua kabisa ni kiasi gani Wanadamu wemeshurutiswa kukubali tu mambo kama kama wanavyoyakuta bila kushangaa, bila kushangaa ni jinsi gani na kwa nini.
Ni muhimu kufanya hivyo na kisha kuendelea na swali kubwa linalofuata, “Kwa nini Mungu kwa ufanisi awaweke watu wasiojua duniani, na kisha anatarajia wao kutambua Asili yao ya kweli na baadaye kurudi kwa Mungu?”
Watu wengi hawana ufahamu huu na hupitia maisha kabisa kwenye giza la Kiroho hadi mwisho wa siku zao kama walivyoanza maisha yao, kwenye Ujinga wa Asili yao ya Kiroho. Jibu la swali hili, kama kawaida, ni kuwaambia watu kwamba njia pekee ya kweli ya kujua (jibu) ni Kutahajudi na kupata Njia ya Kweli ya ndani ya Mwanga na Sauti.Tangu mwanzo wa wakati imekuwa hivyo. Mimi nazungumzia juu ya wakati kabla ya maarifa ya ustaarabu wowote uliopita.
Ulimwengu, na Galaksi zake zote pamoja na Nyota zina siri na maajabu mengi ambayo hatua kwa hatua yanayojitokeza na kugunduliwa. Lakini bado kuna masafa ya kwenda wakati uko kwenye hali na umbo la kimwili. Hata hivyo, kama mtu akifanywa kuwa na Ufajamu wa Kiroho kwa Kutahajudi kisha anaweza “kutembea” kwenye Uumbaji na kugundua mwenyewe siri na maajabu haya. ”
Novemba 20, 2016
Sisi ni Mabwana wa Mwanga.
Jinsi mambo yanavyoendelea, Sisi katika ulimwengu wa Kiroho na nyie duniani lazima kuwa na ufahamu wa mabadiliko ambayo yanahitaji kufanyika, kama Lightwave hii itakuwa na matokeo ya mwisho Tunayotamani. Yaani kubadilisha Ufahamu wa Sayari kwa kuwa na Kuanzishwa kwa watu wengi (mass Initiations), kupata kiasi kinachohitajika cha Mwanga wa Kiroho na Upendo kwa Dunia.
Tumeachilia kiasi kubwa sana ya Nguvu ya Kiroho, zaidi kuliko hapo awali katika miaka ya hivi karibuni.Labda sasa ni wakati wa kulenga Mabara mengine na kueneza Nguvu kidogo zaidi. Kwa njia yoyote, hii sio kuwatelekeza watu lakini kushinikiza mipaka na kuchukua Lightwave katika pande nyingine pia.
Kuna Adepts wa kutosha sasa Amerika ya Kusini ambao wanaweza kufanya kazi wenyewe na Kuanzisha (Initiate) na kuwafanya watu kufahamu nafasi ya pekee ambayo ipo.
Jinsi ambavyo Elimu ya Kiroho daima inafanya kazi ni kuwapa Binadamu nafasi ya kuleta Amani na Upendo kwa kila mmoja wao. Pia kuleta Maarifa ya Ngazi za juu na kuwachukua na kuwatoa watu kwenye hali ya mambo ya kimwili ambayo yapo.
Nafasi hii ipo SASA – tafadhali Tusikilizeni.
Novemba 18, 2016
Sisi tunatumaini ni mara ya kwanza ya mengi wakati Tunaona kwamba watoto Wakitahajudi kwenye umri mdogo haitakuwa nzuri tu kwa ajili yao na familia zao, lakini pia wao watakua na kuwajibika kwao wenyewe na si kutegemea watu wengine kwa furaha yao na usalama. Wao watatambua kwamba furaha na usalama hutoka ndani mwao wenyewe, kwa ndani.
Sisi tuna furaha kwamba watoto hawa wanaweza kuonyeshwa kwamba kuweka muda wa dakika chache kila siku kwa Kutahajudi kutaleta matokeo ya kushangaza, ikiunganishwa pamoja na kutuma Upendo kwao wenyewe, familia zao na marafiki na kwa Sayari itawasaidia kufahamu kwamba wao ni sehemu ya harakati za kuunganisha Dunia kwa amani.
Hebu watoto waonyesha njia kwanza kwa kuwa na ukarimu na upendo kwa kila mmoja wao, familia zao na jamii zao ambao utaenea kwa Nchi na kisha Dunia nzima.
Upendo ndio Ufunguo.
Oktoba 24, 2016
Sisi tunafurahishwa sana kuona Adept wote na Walioanzishwa (Initiates) ambao hukusanyika pamoja kusherehekea kwa Upendo na kuthamini Zawadi ya Kiroho waliyoipata.
Kama mnagawana kile mlichokuwa nacho mtahamasishana wenyewe zaidi. Kuna Maajabu yasiyo na mwisho ya kuchunguza katika Tahajudi zenu. Enlightenment ni mwanzo mpya, una fursa sasa sio tu ya, daima kubadilisha maisha yako kuwa mazuri zaidi, lakini kwa kuwa muhimu katika kubadilisha maisha ya watu wengine wengi pia.Hii ni wakati kwa ajili ya ukuaji Elimu ya Kiroho kwa Sayari ambayo kamwe haijatokea. Amani na Furaha iwe kwenu wote.
Oktoba 12, 2016
Sisi ni Viumbe wa Mwanga tunataka kuzungumza nanyi kuhusu huduma.
Ni muhimu kukumbuka neno hili katika maisha yenu ya kila siku. Kwa kuwa umeanzishwa (Initiated) kwenye Njia ya Kiroho watu wanakuangalia na kukutegemea kwa ajili ya kuwahamasisha na msukumo na pia kuwa na asili ya kutoa.
Service ina maana ya uendelevu wa kutoa – kutoa kunakoendelea bila kujali kitakachotokea – wakati mwingine bila shukrani na kuthaminiwa.
Ukiwa na Mwanga na Sauti una zana zote unazohitaji kuishi maisha yako kwa njia ya kutosheleza na furaha zaidi. Tunajua hii sivyo ilivyo kila mara, lakini kama Unatahajudi kwa Upendo na shukrani kwa kile ulicho nacho, mabadiliko ya ajabu yanaweza kufanyika. Unatambua zaidi na zaidi Asili yako ya Kiroho, ambayo hukusaidia wewe kuelewa matatizo ya duniani na jinsi ya kukabiliana nayo.
Oktoba 11, 2016
Kuna kile kinachojulikana kama Mwalimu (Master Principle) kama mnavyojua. Wakati inapotokea haja basi Kiini (Essence) kitakuwa “chaji” ya Mwalimu kanuni (Master Principle).
Kiini hiki kinahitaji kuchaguliwa kwa makini na kinaweza kutumika tena na tena kama hali ikijitokeza, wakati ni muafaka kuwasaidia Binaadamu.
Unaweza kuona kwamba wakati mwingine mwili wa Mwalimu hufanya kazi tofauti kuliko wengine. Kama Kiini Kilichochaguliwa kikifanya kazi kwa mujibu wa mpango basi mwili unaonekana kuwa na mafanikio. Kila Mwalimu ana mamlaka mbalimbali.
Hii Lightwave mpya inazidi matarajio yetu – lakini tunawaonya – itabidi kufikiria upya jinsi itakavyofadhiliwa, kwani mtahitaji fedha kwa kutuma watu Nchi mbalimbali, japo sio fedha kwa ajili ya kuanzisha (initiations)!
Oktoba 2, 2016
Kinatokea ni kikubwa hakijawahi kutokea, hamjatambua jinsi gani yote hii ni ajabu na jinsi ambavyo Uwezekano wa Kweli unaongezeka zaidi kila siku.
Jinsi ambavyo wote Mnatahajudi kwenye Mwanga na Sauti hii inachaji na kubadilisha Sayari nzima – kutoka kwenye msingi wake hadi bahari zote, milima, mito, wanyama na Binadamu. Vyote vinaathirika kwa njia nzuri.Bila kujali kuwa Nguvu hii inatoka wapi ili mradi Walioanzishwa (Initiates) Wanatahajudi kutoka ndani ya Mioyo yao – 75,000 wa kwanza watatoka Marekani Kusini lakini kutakuwa na Watahajudi kutoka sehemu zote za dunia.
21 Septembet 2016
Tunahitaji kuzungumza na nyie kuhusu mitazamo mizuri. Mengi zaidi yanaweza kupatikana kwa kuishi maisha yenu kwa njia hii. Tunajua kwamba sio matokeo yote ni mazuri, lakini hiyo inaweza kuwa kwa sababu ya masomo yanayo hitajika kujifunza. Kubali na endelea!
Uko hapa kuwa na Furaha na kuleta Furaha nyingi kwa wengine kama iwezekanavyo. Kuleta furaha kwa watu wengine ni kuleta Furaha kwenu wenyewe. Weka tabasamu kwenye uso wako na kuwapa watu wengi kama unaweza.
Sisi tuko pamoja nanyi siku zote hata kama nyie hamna ufahamu kuwa tupo. Hakuna mtu milele yuko peke yake, hata wakiwa katika muda mbaya sana.
Unachotakiwa kufanya tu ni kuomba msaada wetu – utaona, Maajabu yakitokea!
Septemba 18, 2016
Hii ni habari ya kusisimua kuhusu Mabadiliko Makubwa yanayokuja. Humuwezi kuiona kwa ukamilifu wake k.m. jinsi dunia itakavyokuwa – lakini hakika mnaweza kuamini kuwa itatokea.
Tunahitaji watu ZAIDI kubadili mawazo yao na kuamini kuwa kinachoendelea ni HALISI na dunia itapungua kuwa ya kimwili na kwa ujumla kuwa ya furaha zaidi.Ni rahisi sana Kwetu sisi kuwaambia huu Ukweli wa Milele:
Upendo ni Muhimu (ndio Ufunguo)
Upendo ni jibu la maovu yote
Upendo unaweza kushinda vizuizi vyote
Jinsi watu zaidi ambao wanaweza kuleta Upendo katika maisha yao, ndivyo Dunia itakavyokuwa bora zaidi, pamoja na watu binafsi pia.
Sisi tuko hapa kuleta MATUMAINI Duniani kwani sisi tunaona kuwa matumaini yamepotea kwa watu wengi. Ikiwa hakuna matumaini, watu huacha hata kujaribu kupigania haki zao, uhuru, utu wao na kujithamini.
9 Machi 2016
Huu ni ujumbe kwa wote ambao wanataka Initiation, au States zaidi kwa maendeleo kwenye Njia kupata Enlightenment.
Sisi hapa tunaona maandalizi mengi yanayoendelea na inatutia moyo sisi kwa sababu ina maana kwamba Nguvu zinazotumwa zitatumika vizuri, na kwa dhamira inayostahili.
Ninyi, kama watu mnaotaka Kuanzishwa (Initiation) mnaweza kuwa na uhakika kwamba katika kila hatua ya safari mtakuwa mnatunzwa, kusaidiwa na Kupendwa na Sisi.
Ni Safari ya kujua kuhusu maswali makubwa ambayo unaweza kuwa unatafuta maisha yako yote. Kwa mfano, ‘Kwa nini tuko hapa? ”
Labda utakuwa umetafuta majibu katika vitabu vya kiroho na kukatishwa tamaa.
Kwenye hii safari ya Mwanga na Sauti utapata majibu mwenyewe. Kutakuwa na haja ya ufafanuzi kwani wewe utajua katika moyo wako kuwa majibu ni Kweli; yote yataleta maana kwako.Unaweza kugundua kuwa wewe unafikiri kwa njia tofauti, mawazo ya zamani na jinsi ya kuwa, chakula, n.k. vitabadilika. Hii yote ni utaratibu wa kawaida wa “Kuachia” na kuwa na uwezo wa kuwa bora kama unavyoweza kuwa wakati uko kwenye mwili wa kimwili. Kufikia Hali ya Kiroho ya juu kabisa wa Enlightenment – ambayo, kwa upande wake itakusaidia kuongeza uelewa na ufahamu wa binadamu wenzako.
Februari 10, 2016
Sisi ni viumbe ya Mwanga ambao ni udhihirisho halisi wa Upendo bila masharti. Sisi sio Enlightened kama wewe kwani hatuna mwili wa kimwili (physical body) ambao ni muhimu ili kuwa Enlightened.
Sisi Tuna Upendo kwenu na tunafahamu mateso mengi yalioyoko duniani. Hatuhisi mateso, kwani Nguvu yetu, ulinganifu wetu ni wa juu, lakini sisi hutambua kuwahurumia na tungependa kusaidia. Njia ambayo tunaweza kufanya hivyo ni kwa kuwasaidia kuongeza Ufahamu wa pamoja wa Dunia. Hii itafanikishwa kwa watu wengi iwezekanavyo Kutahajudi kwenye Mwanga na Sauti na kuwa Enlightened. Hivyo tuna vipindi kadhaa vilivyopangwa vya Neema kwa Wote, ikiwa ni pamoja kipindi kirefu wakati wa Pasaka, wakati Neema inaruhusu mabadiliko ya Hali za Kiroho.
Sisi tuna msisimko sana kuhusu idadi ya watu ambao watapata Mwanga na Sauti, na wale ambao watapanuka kutoka Initiate wa Kwanza kwenda Initiate wa Pili Initiation na bila shaka Enlightenment. Matumaini yetu ni kwamba wale wote ambao watafaidika watakuwa, kwa njia ya Upendo, kusaidia wengine kufuata Njia huu na kufikia Enlightenment. Kwa kufanya hivyo mtakuwa mnaongeza Ufahamu ya dunia hii na wakazi wake.
Ongeeni nasi. Wasilianeni Nasi na tutawaongoza na kukusaidia. Tumieni Uwiano wa Kiroho tuliowapa kuponya kila mmoja wenu. Upendo hauna na haujui mipaka. Onyesheni Upendo kati yenu na kwa Binadamu na Dunia na kuheshimu jamii ya wanyama.
Januari 16, 2016
Nguvu na Uzuri wa Mwanga na Sauti kwa watafutaji wote wa kweli ni kubwa na zaidi ya elimu ya kila Binadamu. Ni katika Kutahajudi tu kwa njia hii ambapo Ukweli juu ya Maumbile unaweza kupatikana. Kila mtu ana uwezekano na uwezo wa kutambua Nguvu hii; ni kwa njia ya uvumilivu na kujitolea kuwa Maarifa haya yatatolewa kwao.
2 Januari 2016
Kuhusiana na ubongo na jinsi unavyofanya kazi – hautumiki kiasi cha kutosha na sababu ni kuwa tangu Binadamu amekuwa Duniani kumekuwa na mabadiliko makubwa ya jinsi ambavyo ilitumika.
Tangu Binadamu alivyoishi katika hali ya kale mpaka sasa kumekuwa na mabadiliko mengi na ubongo umebidi kubadilika kulingana na mabadiliko haya. Sisi tunazungumzia juu ya kupanda na kuanguka kwa ustaarabu na Elimu ya Kiroho imechangia kiasi kikubwa. Kwa hiyo, bila shaka sehemu hiyo ya ubongo iliyowajibika kuunganisha na Ngazi za juu za Ufahamu ilikuwa ikitumika mpaka kuanguka kwa ustaarabu unaohusika. Kisha ikawa haitumiki na kukaa bila kufanya kazi.
Inabidi kutambua tu, kwamba kila ustaarabu mkubwa imehusishwa kwa namna fulani, kwa kiwango kikubwa au kidogo na Maisha ya Kiroho.
2 Januari 2016
Wakati Binadamu kwa mara ya kwanza alipokuwa na utambuzi wake mwenyewe kwa namna ya Ufahamu zaidi yeye moja kwa moja alimtafuta “Muumbaji” wake na sababu za kuwepo kwake. Tulikuwa tayari wakati huo kumpa majibu aliyohitaji.
Kama mnavyotambua, dini zimeibuka kutoka kwenye “ujumbe uliotoka juu”, ambazo zilikuja na kutoweka kwa muda wa karne nyingi. Hii ndiyo sababu kuna kufanana kati ya imani na dini, kwa sababu kwenye Chanzo ujumbe huo ulitumwa kwenda kwa “wasikilizaji” waliokuwa tayari. Ni jinsi gani ingekuwa vingine, kuna Ukweli mmoja tu.
Kuyaandika haya itasaidia watu kupata baadhi ya ufahamu wa jinsi Roho inavyofanya kazi. Itawapa watu njia wazi zaidi ya kutafuta “Lengo” lao, ambayo haipo katika Dunia kwa sasa.
Septemba 17, 2015
Sisi tayari tulishasema kuwa Upendo ni kanuni ambayo imeenea kwenye vitu vyote na kila kitu kilichopo kipo kwa sababu Yake. Kama hivi ndivyo ilivyo kwa nini kuna vita viingi katika dunia? Je hii si inaenda kinyume na asili ya kweli ya Mtu? Kwa nini katika Dunia iliyopo kwa sababu ya Upendo kwamba kunaweza kuwa na Chuki kiasi hiki?
Jibu liko kwenye pande mbili (duality). Nje na ndani, nzuri na mbaya, juu na chini, upendo na chuki. Misheni ya Mtu ni kuwa zaidi ya asili yake ya pande mbili duniani, Kutahajudi kwenye Mwanga na Sauti ambayo itamwonyesha njia ya kupata Upendo kwenye Enlightenment ambao hauna kinyume.
Upendo upo wenyewe, bila masharti, bila kingo, bila mipaka.
Hakuna hukumu kwenye Upendo.
Upendo ni msamaha na hauhitaji ………
Upendo unakubali vitu vyote kama vilivyo.
Upendo unaopatikana kwenye Enlightenment ni Safi, usio na dosari, na hauwezi kuathirika au kuchakachuliwa.
Upendo ni haubadiliki daima.
Furaha ya kweli ni Upendo wa milele.
Upendo ni Kielelezo cha Mwisho cha Ukweli. Haukatai chochote na inatoa kipaumbele kwa kila kitu.
Nini ni kizuri zaidi kuliko Upendo upatikanao kwenye Enlightenment?
Upendo ndiyo kitu pekee ambacho hakiwezi kudhibitiwa. Upendo una kila kitu; Upendo unasaidia kila kitu.
Upendo ni Kielelezo cha Mwisho cha Umoja wa Ulimwengu (Universal Oneness).
Agosti 27, 2015
Upendo ni Nishati isiyo na Mwisho ambayo imeenea kwenye Maumbile yote. Kila mahali unapoangalia kuna Upendo, kwa sababu kila kitu unachoweza kuona, kuhisi na kugusa kipo kwa sababu ya Upendo. Kila kitu kinashikamana, hivyo kila wazo, tendo au neno liko kwenye kumbukumbu.
Hakuna kitu kinachopotea: maneno yaliyosemwa kwa hasira yana nguvu zaidi na yanasababisha madhara zaidi kwa hiyo jaribu kuwa mpole zaidi jinsi unavyofanya mambo yako. Angalia na dhibiti hisia zako na fikiria kabla ya kuongea.
Agosti 27, 2015
Hii itaeleza matatizo ambayo watu wanayo katika mahusiano yao ya karibu:
Wakati unachukua mwili (incarnation) mara zote kuna masomo ya maisha yaliyopangwa kabla ya kuzaliwa. Haya yanaweza kuwa kitu chochote kutoka kujifunza kuhusu uhusiano mbaya, mtoto kufariki au tu kwa ujumla kukabiliana na heka heka za maisha. Watu wengi wanaona ni vigumu kukabiliana na chati (patterns) ambazo zinazuka katika maisha yao. Mara tu wakielewa kwamba hivyo ni vielelezo ambavyo hujitokeza kwenye “mifumo” yao, basi watakuwa na furaha na afya njema zaidi. Watu wengine wapo kuwaonyesha baadhi ya mambo kwenye maisha yao wenyewe na wanavyozidi kupinga ndivyo yanavyozidi kujitokeza.
5 Mei 2015
Hali ya kudumu ambayo mnaisema haiwezi kuwa ya kudumu, katika mwili wa kimwili. Unaweza kuwa na Utambuzi na Hali za Ufahamu lakini hivyo ndivyo zilivyo, sio hali ya kuwa.
Kwa mfano, unaweza kushuhudia hali ya “kuto-kufikiri” kwenye Tahajudi ya kina, lakini wewe ni shahidi, sio hali.
Kwenye Enlightenment unakwenda kwenye ile “hali ya kudumu” kwa muda, unajisikia tofauti na maisha yako itabidi kubadilika – lakini unarudi kuishi maisha yako, angalau kwa mtazamo tofauti. Narudia tena, wewe UNARUDI, inabidi, ama sivyo hutaweza kufanya kazi kama binadamu.
Mtu aliyekuwa Enlightened akifa anaachia kwanza gamba lake wa kimwili, anapanda kwenye ngazi za juu za maubile na kuingia kwenye “usingizi mkubwa” na kuendelea kuachia miili zaidi ambayo ilitumika wakati akiwa kwenye umbo la kibinadamu duniani. Kisha mabadiliko hutokea na “yeye” tena sio “mtu binafsi” lakini bado ana ufahamu, Kiumbe wa Mwanga. Kiumbe wa Mwanga kisha anajiunga na Kiini chake ambacho daima kinaishi kwenye Ulimwengu wa Kiroho ..
Kinachofuatia hii kuna mambo matatu yanawezekana:
1. Kuunganika kwenye Umoja…….daima.
2. Kukaa na kubaki kwenye ulimwengu kiroho, kuhudumia na kuendelea kujifunza.
3. Kurudi kwenye ngazi za kimwili kwa kuchukua seti nyingine ya miili kwa ajili ya kufuatilia zaidi masomo ya maisha.
Aprili 27, 2015
Mawimbi ni sehemu ya utaratibu wa maisha na nguvu zote zinaweza kuchukuliwa kama kuwa asili ya wimbi. Mawimbi pia yanakuja kutoka ngazi za juu, wakati dunia iko tayari, kuleta mabadiliko ya mageuzi. Hizi ni pamoja na “cheche” ambazo husababisha uvumbuzi mpya na teknolojia pamoja na mawazo mapya ambayo yanatolewa wakati Binadamu amebadilika kwa kiwango fulani ili awe na uwezo wa kuyapokea mabadiliko haya.
Mzunguko ni muhimu kwa sababu ya asili ya Mtu. Yeye anahitaji muundo ili kuishi, lazima kuwe na utaratibu katika maisha ya watu. Kila siku jua linachomoza na kutua kwa wakati wa kutabirika kama ambavyo misimu hurejea kutoka mmoja hadi mwingine. Baharini maji hujaa na kupwaa kwa usahihi wa hisabati na wanawake kuonyesha mzunguko wa hedhi ambayo inahusiana na nyakati za mwezi. Dunia katika zamu za kuzunguka mara moja kwa siku, inazunguka Jua kufafanua mwaka na mara kwa mara huyumba kwenye mhimili wake. Hata kupumua kwetu na mipigo ya moyo ni “rhythmical”.
Haya yote kuongeza utulivu wa Mtu ili kukabiliana na heka heka za kuishi tu.
Aprili 26, 2015
Jibu lako lipo si kwenye jinsi ya kuondoa (nia ya vita) lakini jinsi ya kubadilisha ufahamu wa Sayari yako. Mara baada ya tamaa ya madaraka inapogeuka kuwa uvamizi hakuna mengi ya kufanya. Sisi tunachokusudia kufanya ni kwenda kwenye chanzo cha akili ya binadamu kujaribu kuondoa hii asili ya kupenda madaraka.
Siku zote kutakuwa na viongozi wa dunia ambao wanalazimika kufuata mahitaji ya wale wanaowatumikia. Sisi tunachozungumzia ni watu wa kawaida ambao wanachafuliwa na kile mnachokiita “Dunia ya Kisasa”, ambayo kwa wakati huu ina maana uvamizi mkubwa wa Teknolojia Mpya ambayo inadumaza mawazo ya watoto wenu ambao ni watu wazima wa baadaye.
Nini kinaweza kufanyika? Naam, katika ngazi ya Kiroho tunaweza kuongeza ufahamu lakini msiidharau nguvu ya taswira. Haihitaji watu wengi kiasi mnachofikiria kuwa pamoja kama akili ya pamoja kuwa na taswira ya maeneo yenye vita na kuchukua nafasi ya hofu, chuki na kutafuta madaraka kuwa upendo na msamaha.
Mawazo ya Mtu binafsi yana nguvu sana: nini kingetokea ikiwa kama watu wenye akili sawa watajiunga kwenye pambano la pamoja kwa ajili ya wema? Unaweza kuanzisha harakati hizi na kundi lako la Watahajudi.
14th April 2015
1. Baada ya kufikia lengo lako lingine daima litatokea. Kwa hiyo usifanye kitu kuwa lengo kama unatafuta ‟Enlightenment”.
2. Malengo ni adhabu kwenye uwanja wa maisha. Yanakuhadaa na kukughilibu kucheza mchezo.
3 Muda ni udanganyifu kuwa sisi tunaenda polepole mno.
4. Usitarajie chochote na Vyote vitafunuliwa.
5. Mwelekeo husababisha mgawanyiko: bila mwelekeo inaongoza kwenye ‟Enlightenment”.
6. Mto unapita lakini bado upo.
7. Hapo mwanzo kulikuwa na Neno: kabla ya mwanzo kulikuwa na Ukimya. Hapo mwanzo kulikuwa na Mwanga: kabla ya mwanzo kulikuwa na Giza.
8. Mtazamo wetu kikomo chake kinategemea uwezo wetu wa kuoana na Ukweli.
9. Kuwa katika mawazo kunatuweka duniani: kuwa nje ya mawazo kunatuweka mahali pengine.
10. Kuwa ndani ya mipaka huleta usalama: kuwa nje ya mipaka huleta Uhuru.
11. Usitoe ili uweze kupokea: Daima pokea ili uweze kutoa.
12. Ukimya hauwezi kupatikana kwenye sauti: lakini Sauti inaweza kupatikana kwenye Ukimya.
13. Giza haliwezi kupatikana kwenye mwanga, lakini mwanga unaweza kupatikana kwenye Giza.
14. Mwisho na mwanzo ni utenganikaji wa mawazo.
15. Tunapoangalia kwenye mwelekeo wowote mmoja tunakosa Kila kitu.
16. Sababu ni mwanzo tu wa kile kilicho.
17. Kile kilicho, kipo: kile kisichopo – ni Mungu.
18. Wakati maarifa yanatoa njia kwa kukubalika – Ukweli una nafasi.
19. Jibu linafunuliwa wazi wakati kuhoji kunaposimama.
20. Kujua ukweli ni kutojua: Kutojua kabisa ni Ukweli.
21. Mwishoni hakuna mwanzo: Mwanzoni hakuna mwisho.
22. Tunapoishi tunakufa: wakati tunakufa Tunaishi.
23. Kama ukiheshimu kila kitu karibu na wewe utagundua kwamba Kila kitu kinakuheshimu wewe.
24. Hebu nafsi iwe kweli na shukurani ili shukrani iweze kuifunua Nafsi.
25. Kioo huonyesha nafsi ikiangalia Nafsi na kisha inaonyesha kioo kuwa udanganyifu.
26. Utupu ni udanganyifu tu wa Uwezo.
27. Rangi hutokea wakati mwanga unayeyuka na melodi wakati Sauti inayeyuka… vyote ni vielelezo vizuri vya Umoja wa Milele.
28. Tunapotoweka tunakuwa Kila mahali.
29. roho ya Kiini ni kiini cha Roho.
30 Kama ilivyo Juu, ndivyo ilivyo chini: moja ni picha ya Nafsi, nyingine nafsi iliyojitokeza kama Umoja milele.
31. Muda hausubiri mtu yeyote; bali hatimaye hakuna mtu unayeweza kusubiri muda: Ni udanganyifu tu ambao tunatumia kupima mabadiliko.
32. Kadri tunavyosafiri mbali zaidi ndivyo tunavyoacha vitu vingi zaidi nyuma. Kwa hiyo tafuta mahali fulani ambapo haiwezekani kusafiri, hivi kwamba kusiwe na kitu tena cha kitapotea.
33. Wazo ni fremu moja kutoka kwenye filamu ya maisha. Usinaswe na kuishia kwenye mchezo tu: mtafute Mwandishi!
Huduma kubwa kuzidi zote ni kuleta Roho kwenye Udongo “matter”.