“Ascension”

Mengi yameandikwa kwenye maandiko ya dini na ya mafundisho ya siri kuhusu Ascension. Pia tunawasilisha ujumbe kutoka kwa Uongozi wa Kiroho ambao unatabiri hali kama hiyo.

Je, inawezekana kufikiria ni jinsi gani mabadiliko hayo yatakavyokuwa? Jibu rahisi ni HAPANA! Tunaambiwa kwamba Ascension hutokea kutokana na ongezeko la mzunguko wa ‟vibration”. Hii inaonyesha kuwa njia tunayoweza kuona mazingira yetu inngebadilika sana. Ingekuwa kama tunaweza kuona rangi mpya na kusikia sauti mpya; tungeweza kuwa nyeti na seti mpya ya Nguvu. Hizi ni dhana ambazo hatuna njia ya kuzingatia na kuzifikiria.

Kila kitu ambacho tumepokea kutoka kwa Uongozi wa Kiroho kimeonyesha Upendo na Huruma. Tuliuliza juu ya jinsi ambavyo ‟Ascension” itafanyika na tulikuwa na wasiwasi kuwa baadhi ya watu wangeweza kuachwa nyuma. Walituhakikishia kwamba mchakato huo utakuwa mpole na wazi kwa kila mtu.

“Ni kana kwamba Binadamu ameinuliwa kwa namna fulani, kuwa na uwezo wa kuendelea na maisha yao kwa Nguvu zilizoimarishwa. Ina maana tu kwamba watu Wata ‟Ascend” kweli tu ikiwa wako tayari na itakuwa ni uteuzi wa kibinafsi.”

Kwa hiyo, ujumbe unaonyesha kuwa watu fulani watafanya mabadiliko mara moja na kujikuta katika ulimwengu ambao ni uleule na bado unaelewaka tofauti kabisa. Wao kwa kawaida watawaambia wale walio karibu yao kuhusu kilichotokea. Kwa hiyo ni juu ya watu hawa kuamua kama watachukua hatua zinazotakiwa.

Ni wajibu wa Watahajudi wa Mwanga na Sauti kuhamasisha watu wengi iwezekanavyo ili waweze Kuanzishwa kabla ya Ascension. Pia ni wajibu wetu kuwasaidia wale ambao hawajaanzishwa kufanya hivyo baada ya tukio hilo la Ascension kufanyika.

Kwa Uelewa mpya utakao ongezeka, maisha kama tunavyoyajua kwenye Sayari hii yatabadilika milele. Inapaswa kuleta upungufu mkubwa katika migogoro ya Binadamu. Tunapaswa kwa kawaida na kiasili kutaka kuhifadhi amani kwa kuonyesha Upendo kwa Binadamu wenzetu pamoja na viumbe vingine vilivyopo katika ulimwengu wetu mzuri.